CRDB YAWEZESHA WATEJA HUDUMA ZA BENKI MKONONI

 


📌DOTTO KWILASA

KUFUATIA kukua kwa teknojia ya Mawasiliano nchini,Benki ya CRDB inaendelea kufanya maboresho ya huduma zake ili kukidhi mahitaji ya Wateja wao kulingana na wakati.

Moja Kati ya huduma hizo ni kuwawezesha wananchi  kufungua akaunti ya benki hiyo kwa kutumia simu ya kiganjani popote  alipo na kuepusha usumbufu.

Hayo yameelezwa Jijini Dodoma na  Meneja Mafunzo na Maendeleo ya Benki hiyo Edith Mwiyombela wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonyesho ya pili ya elimu na Ufundi mabayi  yaliyoandaliwa na Baraza la elimu Tanzania(NACTE) yanaendelea katikaViwanja vya Jamhuri.

Akiongea katika maonyesho hayo alisema hivi sasa wamefanya maboresho katika huduma za kifedha na kuwa rahisi ikiwa ni pamoja na kupunguza masharti kwa wateja .

Alisema,huduma hiyo itaondoa vikwazo ambavyo wateja wengi huona kama kero kwao ikiwepo barua ya wadhamini ,barua ya Mtendaji,picha ya paspoti pamoja fedha ya papo kwa papo ambapo kwa sasa unaweza kufungua akaunti kisha ukahamisha fedha kutoka kwenye mitandao ya siku kwenda kwenye akaunti.

Huduma hii imerahisisha sana,kwanza mteja atakuwa ameokoa muda ,wateja wengine walikuwa wanatamani sana kufungua akaunti lakini walikosa muda,wakati mwingine walitumia muda mwingi katika kutimiza vigezo au kukosa kabisa

Kwa upande wake Simon Mukajanga ambaye ni mshirika wa programu ya uzamili katika benki hiyo alieleza vigezo na masharti vya kufanikisha kujiunga na huduma  hiyo ya kufungua Akaunti kwa kutumia simu ya mkononi bila kufika Ofisi za Benki ambapo alisema mteja atatakiwa kujisajili kwa kutumia namba ya kitambulisho cha uraia(NIDA).


Pamoja na hayo alifafanua kuwa huduma hiyo ina faida kwa kuwa inatoa risiti kwa njia ya simu ili kumrahisishia mteja kuwa na kumbukumbu ya miamala aliyoifanya na kuifanyia mipango katika maendeleo yake.

“Risiti inasaidia mtu kupangilia mipango yake katika matumizi,tunawashauri wananchi kuitumia huduma hii kwani inaokoa muda kwa kuwa huhitaji kusafiri ,utatumia simu yake huku akiendelea na mambo mengine ya uzalishaji,”alisistiza.

 SOMA HII PIA:RAIS MWINYI AKUTANA NA SAKHO WA CRYSTAL PALACE,AMPONGEZA

Post a Comment

0 Comments