📌MWANDISHI
WETU
MKUU wa Jeshi la Polisi
nchini IGP Simon Sirro, ameutaja mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni kama kinara wa uhalifu nchini ambapo
matukio ya uporaji, uvunjaji wa kutumia nguvu na uporaji kwa kutumia pikipiki
yakiwa yameongezeka huku uhalifu mwingine mkubwa wa kutumia silaha za moto
ukiwa umeshuka.
IGP Sirro amesema hayo
jijini Dar es salaam, wakati akizungumza na Wenyekiti wa Serikali za Mitaa,
watendaji Kata, pamoja na watendaji wa vikundi vya ulinzi shirikishi ambapo
amewataka watendaji wote kutimiza wajibu wao kwa kuhakikisha usalama unaendelea
kuimarishwa.
Aidha, IGP Sirro ametoa muda
wa wiki moja kuhakikisha wanakomesha vitendo vya kihalifu kwa kushirikiana na watendaji
wengine huku akitoa wito kwa mgambo kuacha kujiingiza kwenye vitendo vya
rushwa.
Watendaji wa Kata na Wenyeviti wa Mtaa wanajukumu la kuhakikisha Ulinzi na Usalama katika maeneo yao unaimarika.Kama hali ya uhalifu inashamiri hakuna haja wao kuendelea na nafasi hizo
IGP Sirro
ANGALIA TAARIFA KAMILI👇👇👇
0 Comments