IONGOZI WAPYA TUCASA UDOM WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KUONESHA NJIA




📌FAUSTINE GIMU GALAFONI

HAYO yamebainishwa  jijini Dodoma  mwishoni mwa Juma lilopita na Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa chuo Kikuu cha Dodoma,Mch. Bunga Edward Dettu katika makabidhiano ya uongozi Mpya   wa chama cha Wanafunzi Waadventista Wasabato Vyuo vya kati na vyuo vikuu(TUCASA)kanda ya chuo Kikuu cha Dodoma .

Mch.Bunga  amesema  Viongozi  ni wajibu  muhimu kuonesha njia na malengo na mipango kwa maendeleo ya kanisa .

“Vijana wa TUCASA ni nyenzo muhimu sana katika kufanikisha masuala ya utume hivyo katika tukio hili muhimu la kukabidhiana madaraka nimewaasa viongozi wa TUCASA wapya kuonesha njia pamoja na kukabiliana na changamoto katika maeneo ya vyuo maana changamoto zozote ni za kuja na kuzitatua ,hakuna changamoto zinazodumu milele”amesema

Aidha,Mch.Bunga aliwahimiza wanachama wa TUCASA  kuendelea  kuwa wa mfano wa kuigwa kwa watu wengine katika kuonesha njia iliyo bora na impendezayo Mungu kwa kufanya matendo mema .

Mkurugenzi idara ya champlasia na huduma za  vijana kanisa la Waadventista Wasabato jimbo la kati mwa Tanzania(CTF) Mch. Sabato Maseke alihimiza Wanatucasa kuongeza kasi ya utume katika maeneo ya vyuo.

“Mungu ametupatia fursa ya pekee ya kuwa na wanafunzi wenzetu wasiomjua Mungu katika maeneo ya vyuo,kwa hiyo niwaase wanafunzi wa UDOM na Tanzania kwa ujumla  kutumia nafasi walizonazo vyuoni kuwahubiria habari njema za neno la Mungu wanafunzi wengine walio karibu nao”amesema.

 Katika hatua nyingine mkurugenzi huyo wa Champlasia na huduma za vijana kanisa la Waadventista Wasabato jimbo la kati mwa Tanzania[CTF]  alisema tukio la makabidhiano ya Uongozi TUCASA chuo Kikuu cha Dodoma limekwenda sambamba na utunukiwaji wa  vyeti  kwa viongozi wakuu chama cha vijana kanisani[Master Guard] waliosoma kozi ya Msingi huku akiwaasa vijana kujiunga na chama cha vijana kanisani.

Nao baadhi ya viongozi   wastaafu wa  TUCASA waliokabidhi madaraka kwa viongozi wapya  chuo kikuu cha Dodoma  (UDOM ) akiwemo kiongozi wa mstaafu  idara ya Mawasiliano Yohana Zabron   amesema ushirikiano ndio nyenzo Naye Mwenyekiti Mstaafu  Daniel Tumaini ametoa wito kwa viongozi wapya kumtegemea Mungu katika kufanikisha kazi za Utume  pia akibainisha kuwa yupo tayari kutoa ushauri.

Kwa upande wake mwenyekiti mpya wa TUCASA UDOM kwa mwaka 2021/2022 Yusufu Jonas Kitululu alisema atakuwa pamoja na wana TUCASA wote katika kuifanya kazi ya utume  na yupo tayari kupokea ushauri kwa maendeleo ya utume chuoni.  .

Miongoni mwa majukumu ya viongozi wa Chama cha Wanafunzi wa kiadventista Wasabato vyuo vya kati na vyuo vikuu ni kuhakikisha wanaeneza uinjilisti  maeneo ya chuo.

 


Post a Comment

0 Comments