MBUNGE BAHI AHADI KUKAMILISHA UJENZI WA ZAHANATI VIJIJI 10 NDANI YA MIAKA

 


 ðŸ“ŒJOHN BANDA

MBUNGE wa jimbo la Bahi Mkoani Dodoma Kenneth Nollo amesema amejizatiti kupitia mfuko wa jimbo na michango ya wadau wengine kukamilisha ujenzi wa zahanati 10 kati ya 16 zanazohitajika ifikapo mwaka 2025

Akiongea jimboni humo na waandishi wa habari Mbunge huyo amesema kuwa kukosekana kwa huduma za afya kwenye vijiji hivyo 16 kumekuwa kukiwasababishia usumbufu mkubwa wananchi ambao wamekuwa wakienda umbali mrefu kutafuta huduma hiyo

Nollo amesema ndani ya miaka mitatu na nusu kuelekea mwaka 2025 atahakikisha anaondoa usumbufu huo kwa kujenga zahanati katika vijiji 10 ambapo mpaka sasa tayari ameshatoa million 30 kupitia mfuko wa jimbo kwenye vijiji vya Nchinila,Nguji na chikopelo.

Amesema hata hivyo kupitia zaira ya aliyekuwa rais wa Tanzania Hayati John Pombe Magufuli akitokea jijini Arusha miezi michache kabla ya kifo chake alitoa Million 50, kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa zahanati ya Mayamaya ambapo serikali pia imetoa kiasi kama hicho katika vijiji vya Chali na Nchinila.

Hadi sasa kiasi cha million 30, zimeshatolewa toka mfuko wa jimbo kwa ajili ya ujenzi wa zahanati za vijiji vya nchinila, Nguji na Chikopelo huku serikali ikimalizia ujenzi huo kwa million 50 kwa kila kijiji.

Keneth Nollo

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM wilayani Bahi Stewart Masima amempongeza Mbunge huyo kwani amekuwa akijitoa kwenye kuchangia maendeleo ya wananchi kwa hali na mali

Amesema tangu mbunge Nollo aingie madarakani kwa kushilikiana na wadau wengine amekuwa akifanya mengi ya kimaendeleo yakiwemoujenzi wa shule na zahanati pamoja na kukisapoti chama cha mapinduzi kwenye maswala mbalimbali

“Mbunge kwa kushirikiana na wadau mbalimbali amekuwa akifanya mambo mengi ambapo hata sasa tunasubiri mifuko 500 ya Sumenti kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa zahanati katika vijiji vingine”, amesema 

 

 

Post a Comment

0 Comments