RAIS MWINYI ZANZIBAR AKUTANA MWENYEKITI WA TUME YA HAKI ZA BINADAMU

 


📌MWANDISHI WETU

RAIS wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hussein Ally Mwinyi ameipongeza  tume ya Haki za Binadamu na utawala bora kwa kuanzisha mfumo mpya wa kushughulikia malalamiko ya wananchi kwa njia ya mtandao.

Aidha ameitaka tume hiyo kuongeza nguvu na kulipa kipaumbele eneo hilo kwani litaokoa muda wa wananchi katika utatuzi wa kero zao.

Ameyasema hayo jana mjini Zanzibar wakati wa mazungumzo kati ya Tume ya Haki za binadamu ya kwenda kumpongeza kwa kuchaguliwa kuwa Rais na kuitambulisha Tume na majukumu  yake,mafanikio,  changamoto, na kuomba muendelezo wa ushirikiano kutoka kwenye wizara,idara,na taasisi za serikali.

Naipongeza sana Tume hii na  nitashirikiana nayo kwa asilimia mia moja ili kuiwezesha  na kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa katiba.

Rais Mwinyi

 

Naye mwenyekiti wa Tume ya haki za binadamu Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu amempongeza  Rais Mwinyi kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar kwa kuendeleza Serikali ya Umoja wa Kitaifa, ambayo imepata mapokeo chanya kutoka kwa wananchi.

"Nisema tu kwamba  hatua za kufikia uchumi wa blue, ili kuhakikisha kuwa wananchi wa Zanzibar wanafaidika na matumizi stahiki ya maliasili ya bahari kwa shughuli za biashara ya uvuvi, usafirishaji, na kilimo cha zao la mwani , kwa kuimarisha Haki za Binadamu na Utawala Bora na kuongeza dhana ya uwazi,uwajibikaji,ushirikishwaji usawa na ushughulikiwaji wa malalamiko naomba nikupongeze sana Mhe Rais"amesema  Jaji Mwaimu.

Sambamba na hayo amesema wanafurahishwa kuona  wananchi, kwa kuchukua hatua za  kuanzisha mfumo wa kuwasilisha malalamiko moja kwa moja kwa Rais unaojulikana kama SEMA NA RAIS MWINYI (SNRMWINYI).

"Kitendo cha kuanzisha mahakama maalum ya kushughulikia kesi za udhalilishaji,  na utaratibu wa kusikiliza changamoto za makundi mbalimbali kama vile wanawake, wazee, na wenye ulemavu, na kwa kuimarisha mapambano dhidi ya Rushwa kwa kuboresha Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, kwa kusimamia mapato na matumizi sisi kama tume ya haki za binadamu tumefurahishwa sana" amesema Mwaimu

Sanjari na hayo  Tume imetambulisha  Majukumu yake kwa Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na kuelezea ofisi zilipo bapa nchini.

 "Tume ina ofisi Dodoma (Makao Makuu, Unguja, Pemba, Dar es Salaam, Mwanza, na Lindi. Na kwamba Tume inatarajia kufungua Ofisi Mbeya na Tabora,  na nikujulishe Mheshimiwa Rais kuwa Majukumu ya Tume ni kuhamasisha ulinzi na uhifadhi wa haki za binadamu na misingi ya utawala bora kwa kutoa elimu kwa jamii juu ya masuala ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora, 

"Kwa kufanya tafiti na uchunguzi wa malalamiko pale kunapodhaniwa kuna uvunjifu wa haki za binadamu na misingi ya utawala bora  kupendekeza sheria zenye changamoto katika kuzingatia haki za binadamu na utawala bora  kuishauri Serikali juu ya masuala ya haki za binadamu na utawala bora,kushirikiana na asasi binafsi na taasisi za serikali katika kutatua changamoto za wananchi" amesema Mwaimu

Hata hivyo Jaji Mwaimu amesema  kazi ya tume nyingine ni kuandaa ripoti juu ya hali ya haki za binadamu na utawala bora nchini pamoja na changamoto zake, na kuonesha hatua za maboresho  ya  utatuzi wa changamoto husika zilizochukuliwa na serikali.

 

Post a Comment

0 Comments