📌RHODA SIMBA
KATIKA
kuwepo kwa malalamiko ya wananchi kuhusu kupanda kwa gharama za vifurushi
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umeishauri Serikali kuona
haja ya kuangalia upya suala la huduma za vifurushi.
Hayo yamesemwa leo jijini hapa na katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Raymond Mwangwala wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa kikao cha baraza kuu la umoja wa vijana CCM.
Aidha ameishauri Serikali kuona haja ya kuangalia upya suala la huduma za vifurushi kwa kulichukulia kwa umakini ili kuokoa ajira kwa vijana waliojiajiri katika uchumi wa kidigitali.
Sisi kama vijana wa CCM tunaishauri serikali ,vijana wetu wanaelekea kukosa ajira kutokana na gharama kubwa za bando,tunaiomba Serikali yetu tukufu kuona namna ya kuboresha changamoto ya huduma za vifurushi kupitia mitandao ya simu
Kwani uwepo wa gharama za juu katika manunuzi hukwamisha vijana kukua kiuchumi kutokana na wengi kufanya shughuli zao kupitia mitandao ya kijamii,"amesema
Pia
baraza kuu limemvua uongozi Hussen Salehe aliyekuwa mwenyekiti wa UVCCM wa
wilaya ya Moshi vijijini kwa kutokuwa na maadili pamoja na nidhamu baada ya
kupokea mapendekezo yaliyowasilishwa katika kikao cha halmashauri kuu ya CCM ya mkoa wa Kilimanjaro.
"Baraza
kuu lilijiridhisha,Kamati ilijiridhisha na kuona kwamba kwa tuhuma zile na
mapendekezo yaliyotolewa katika kikao halmashauri kuu ya mkoa hivo limemvua
uongozi,
“Hivyo
naagiza mkoa wa Kilimanjaro kutangaza nafasi ya mwenyeki wa uvccm,
katika wilaya ya moshi vijijini”amesema.
Sambamba
na hayo UVCCM pia imeazimia kumuenzi hayati Dkt. John Magufuli aliyekuwa Rais
wa awamu ya tano kwa kuyaendeleza yale yote mazuri aliyoyafanya katika kipindi
cha uongozi wake.
Lakini
pia wamempongeza Rais wa awamu ya sita Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuteuliwa
kwa ushindi mnono huku akiwawataka vijana kuunga mkono jitihada zinazofanywa na
Rais Samia pamoja na serikali yake.
Tutamlinda
,tutamtetea Rais wa chama chetu iwe mvua au jua,pia kwa kuongeza juhudi katika
kufanya kazi na uzalendo katika nchi yetu
Pia
wamempongeza Daniel Chongolo pamoja na wajumbe wote walio chaguliwa kuunda
sekretarieti mpya ya chama chetu,tunaimani kubwa nao,tupo tayari kushirikiana
nao kwa maslahi ya chama chetu kwa kazi nzuri pia tunakiopongeza chama
chetu kwa kazi nzuri ya kusimamia cham,a chetu.
“Sisi
kupitia wawakilishi wetu wa ngazi mbalimabli za maamuzi
tunaendelea kusimamia serikali na hususani kupitia vijana wakiwa
bungeni,kusimamia serikali kuhakikisha inatekeleza ilani ya chama cha mapinduzi
kwa maslahi ya vijana na taifa kwa ujumla.
0 Comments