EWURA YAKABIDHI MASHUKA VITUO VYA AFYA DODOMA

 


📌DOTTO KWILASA

IKIWA ni wiki ya Utumishi wa Umma,Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) imetoa msaada wa mashuka 431 kwenye vituo vinne  vya kutolea huduma za afya vya jiji la Dodoma ili kuboreshà huduma kwa jamii.

Hayo yamesemwa  Jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Mhandisi Godfrey Chibulunje  alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari .

Chibulunje amesema,  mashuka hayo yatakwenda kwenye vituo vya afya vya Makole,Hombolo ,Mkonze na Kikombo jijini hapa.

Hii ni wiki ya Utumishi wa Umma na leo ndio Kilele cha maadhimisho yake,hivyo EWURA tunaadhimisha siku hii kwa kutoa msaada kwenye vituo vya afya vya jiji la Dodoma kama mchango wetu katika kuboresha huduma za afya.

Chibulunje

Naye  Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma Dkt.Endrew Method  akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo wa mashuka amewashukuru Ewura na kuwaomba kuendelea kujitoa kusaidia katika maeneo mbali mbali ya afya.

Amesema kuwa hiyo siyo mara ya  kwanza kwa EWURA kuwasaidia moja kwa moja jamii ,kwani kuna wakati pia waliwasaidia fedha ambazo zilielekezwa  kwenye huduma ya mama na mtoto na kuongeza kuwa mashuka hayo yanakwenda kuchochea utoaji wa huduma  bora kwa jamii.

Katika kituo cha afya Makole ,takribani wakina  mama 120 wanajifungua kila wiki ,hivyo tunapoboresha huduma tunalenga kuisaidia jamii .
Dk.Method

Dkt.Method pia ametumia fursa hiyo kuwatahadharisha wananchi kuendelea kuchukua tahadhali dhidi ya ugonjwa wa corona.

"Nitoe wito kwa jamii kujihadhari na Corona kwa  kuepuka mikusanyiko,kuvaa barakoa na kutumia vitakasa mikono,"amesema.

 

Post a Comment

0 Comments