SHUGHULI ZA BINADAMU ZINAVYOPOTEZA MISITU TANZANIA

 


📌JOHN BANDA

TANZANIA hupoteza zaidi ya Hekta 400,000 za Misitu kwa mwaka kupitia shughuli mbalimbali za binadamu hali ambayo hupelekea mabadiliko ya hali ya hewa ikiwemo ongezeko la joto.

Akizungumza jijini hapa ikiwa ni  maadhimisho ya wiki ya mazingira Meneja wa Mawasiliano Shirika la Uhifadhi wa Mazingira Duniani(WWF) Joan Itanisa alisema elimu inahitajika kwa wananchi ilikudhibiti uharibifu wa mazingira.

“Tunafanya kazi na serikali pamoja na wana jamii kuhakikisha tunarejesha uoto wa asili ambao unaharibiwa na shughuli za binadamu ambapo tumeamua kuanzisha kauli mbiu za  uhamasishaji ili kunusuru na kudhibiti hii hali ikiwemo kuanzisha kampeni zinazolinda uoto wa asili,”alisema Joan.

Joani pia aliipongeza serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia kwa kuendelea kusimamia Rasilimali za wanyamapoli kwa kuhakikisha zinalindwa kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla.

Alisema kumekuwa na ongezeko la wanyamapoli wakiwemo tembo,vifaru na simba hiyo inadhihirisha kuwa matukio ya ujangili yamepungua kwa asilimia 100.

“Natoa pongezi kwa serikali na wadau wa wanyamapoli wakiwemo WWF kwa kuhakikisha wanapunguza ujangili ambao ilikuwa umeshamili lakini sasa umepungua kwa kiasi kikubwa na kusababisha idadi ya wanyapoli kama tembo na faru kuongezeka na kuongeza idadi ya watalii hivyo kuongeza pato la taifa,”alieleza

Kwa upande wake Afisa Ulaghabishi wa Sera za Mazingira WWF Nuhu Salala alitaja madhara yatojkanayo na uharibifu wa mazingira kwa binadamu.

Alisema kama hali ya uharibifu wa mazingira itabaki kama ilivyo sasa inaweza kupelekea ongezeko la joto na mabadiliko ya hali ya hewa na mmonyoko wa aridhi.

“Kama hatua stahiki zisipochukuliwa za haraka ikiwemo kuanzisha kampeni za kupanda miti ilikurudisha uoto wa asili ulioharibiwa basi tunaweza kushuhudia mabadiliko ya tabia ya nchi ikiwemo jangwa, joto kuongezeka, kubadilika kwa majira, na mafuriko,”alieleza

Post a Comment

0 Comments