SERIKALI YAANZA MCHAKATO WA KUTEKELEZA MABORESHO YA SHERIA NDOA YA MWAKA 1971.

 



 

 

📌FAUSTINE GIMU GALAFONI

HAYO yamebainishwa Julai 2,202 jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Geofrey Pinda   wakati akifungua kikao cha kupata maoni  ya wadau  katika mapitio ya sheria  ya ndoa ya mwaka 1971 uliokutanisha Wabunge,Wenyeviti wa Halmashauri ,Wanahabari   ambapo  amesema kumekuwa na udhaifu katika sheria hiyo kwani umri wa serikali ni miaka 18 lakini vifungu vya sheria ya ndoa Na.13 na 17 ya mwaka 1971 vinaruhusu mtoto kuolewa chini ya umri wa miaka 18 .

 

 

Amesema wameanza mchakato wa kutekeleza uamuzi wa Mahakama kuu katika shauri Na.5 la mwaka 2016 na uamuzi wa Mahakama ya Rufani katika Rufaa Na.204 ya mwaka 2017 kuhusu vifungu vya 13 na 17 vya Sheria hiyo vinaruhusu mtoto kuolewa chini ya umri wa miaka 18 kuwa ni kinyume na katiba ya nchi.

Tunaingia kwenye mjadala mkubwa na ninyi tunawashirikisha kama Wanachi wa Dodoma kwaajili ya kupitia na kupata namna ya kuitengeneza hii sheria ,kumekuwa na udhaifu katika sheria hii ,umri unaotambulika na serikali ni 18 lakini kwenye vifungu hivi vinasema anaweza kuolewa chini ya umri wa miaka 18 ambayo ni miaka 14 na 15 kwa majadiliano ama ridhaa ya wazazi

Pinda.

Pinda amefafanua kuwa  inapaswa kutafuta kitu ambacho kitawalinda watoto mpaka pale watakapofikisha umri wa miaka 18’’Unaweza kuona mtihani tulionao tunatakiwa kutafuta kitu ambacho kitawalinda, lakini vipi kwa wale ambao hawasomi tunapaswa kuwalinda pia ili wanapotaka kuolewa wawe wamefikisha umri wa miaka 18’’amesema Pinda.

Pia amesema wakati mwingine watoto huozeshwa katika umri mdogo hali inayopelekea kushindwa kuhimili ndoa wakiwa na umri mdogo’’ ndiyo maana Majaji wametuambia tutafute namna nzuri ya kuwaelekeza hawa watoto,tunahitaji mawazo juu ya sheria hii, tuko hapa kupokea maoni yenu mbalimbali kuhusiana na hii sheria ilil isilete madhara kwa watoto na lazima iboreshwe’’amesema Pinda.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju amesema wanachohitaji ni kupatikana kwa haki ambayo itawasaidia wanachi kupata haki katika mifumo ya utoaji haki ’’tunahitaji Kulinda haki za wanawake na watoto wakike katika mifumo ya utoaji haki hasa kwenye sheria hii ya ndoa,tunachohitaji ni maoni kutoka kwa wadau kuhusiana na sheria hii’’amesema Mpanju

 


Msahiki Meya wa jiji la Dodoma Prof.Davis Mwamfupe amependekeza kuwa mtihani wa Darasa la saba usiwe wa mwisho bali uwe mtihani unaotoa njia panda mtoto mwingine anaenda vyuo vya ufundi na mwingine anaendelea na sekondari.

‘Kwa kufanya hivyo tutamlinda zaidi mwanafunzi na kumwongezea maarifa zaidi’amesema.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chemba Comrade Sambala  amesema si kweli kuwa makabila yote yanalingana maumbile hivyo suala hilo ni la kuangalia kwa upana zaidi.

Mkuu Maendeleo ya jamii halmashauri ya jiji la Dodoma  Sharifa Yusuph amesema kuna haja kubwa kwa sheria kufanyiwa mabadiliko kwani mtoto aliyechini ya umri wa miaka 18 hawezi hata kufanya uchaguzi huku mhariri wa Tanzanite Selina Mathew akisema mtoto chini ya umri wa miaka 18 hawezi kuhimili tendo la ndoa ambapo Mtangazaji kutoka Azam Tv Joyce Mwakalinga akisema ni muhimu sheria  mpya kufanyiwa mchakato mapema.

 Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Antony Mavunde amesema ndoa za utotoni zimekuwa zikikwamisha maendeleo ya mtoto wa kike hivyo anaungamkono uamuzi wa mtoto wa kike kuolewa akiwa na umri wa miaka 18.

 

Naye Mbunge wa jimbo la Mvumi Livingstone Joseph Lusinde amesema ujenzi wa Taifa bora ni lazima uanzie katika ngazi ya kaya.’’hivi ni kweli mtoto haelewi si kweli haelewi ,hawa watoto wanaanza wakiwa na umri gani,tusianzie kwenye sheria tu ni kuanzia ngazi ya kaya ,napata shida sielewi tunataka kupata nini,sheria hii inapingana na mila na desturi,utafiti unasemajie tumefanya ya kutosha kuhusiana na matatizo makubwa tuliyonayo ili nchi ikawe sawasawa,nashauri mila na desturi zetu ziimarishe suala la watu kuoana hata wazazi hawahusiki,tusiweke sheria ambayo itatukosanisha na watu ‘’amesema Lusinde

 

Post a Comment

0 Comments