DC SHEKIMWERI AAGIZA UJENZI WA “GOVERNMENT CITY COMPLEX “ UWE UMEKAMILIKA MWEZI HUU

 

 


📌FAUSTINE GALAFONI


MKUU wa Wilaya ya Dodoma mjini Jabir Shekimweri ameagiza ujenzi wa mradi wa hoteli ya jiji la Dodoma  inayojengwa mji wa serikali Mtumba ijulikanayo Government City Compex Hotel  uwe ukamilika  ifikapo tarehe 31,Agosti,2021.

 

 

Shekimweri ametoa maagizo hayo mwishoni mwa wiki akiwa katika ziara yake ya kukagua maendeo ya ujenzi wa kitego uchumi hicho cha jiji la  Dodoma  ambao umegharimu takriban Tsh.bilioni 18  fedha zitokanazo na mapato ya ndani.

 

Mkuu huyo wa wilaya amesema hoteli hiyo itakapokamilika itasaidia kuingiza mapato ya Tsh.bilioni 1.3 kwa mwaka sawa milioni 108 kwa kila mwezi hivyo unapochelewa kukamilika unapoteza mapato ya Tsh.Milioni 108 kila mwezi na hadi sasa jumla ya Tsh.Milioni 864 zimepotea kutokana na kuchelewa  ambapo ulitarajiwa kukamilika mwaka jana.

 

Vile mnavyochelewa kumailizia ujenzi ndiyo mnavyodhidi kupoteza mapato,kwa sababu hadi sasa mmetoa tu lakini hamna dalili kuirudisha fedha ya wananchi kwa sababu mmechelewa kumaliza ujenzi.




DC Shekimweri akikagua moja ya chumba cha hoteli iliyopo
katika kitega uchumi hicho.


 

Mstahiki Meya wa jiji la Dodoma Prof.Davis Mwamfupe amemuonya mkandarasi wa jingo hilo kuendelea kufanya kazi kwa weledi na ubora hili kitega uchumi hicho kiltie matokeo yaliyokusudiwa na halmashauri ya jiji la Dodoma.

 

 Prof.Mwamfupe alisema uharaka wa ujenzi huo usiathiri ubora wa umaliziaji wa jengo hilo ambalo taratibu zote za malipo kwa mkandarasi zilishakamilika.

 

 Kwa upande wake  mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi [CCM]Wilaya ya Dodoma Meja Mstaafu Johnick Risasi akisema suala la mkataba linatakiwa kuangaliwa upya ili kuondoa mkanganyiko pindi panapotokea ucheleweshaji wa miradi.


Risasi alisema kila upande lazima uheshimu mkataba ili kutumiza malengo ya miradi hiyo kwa muda uliowekwa.
 

Awali akitolea maelezo juu ya mradi huo ,msimamizi wa ujenzi katika hoteli hiyo ya kisasa  mji wa serikali yenye hadhi ya nyota tano,mhandisi Nasri Nasoro  kutoka kampuni ya  M/S MOHAMMED BUILDERS CO.LTD  inayotekeleza mradi huo amesema ujenzi wa Hoteli hiyo umefikia asilimia 75.

 

 

Post a Comment

0 Comments