UHAKIKI : WAZIRI UMMY AWAITA WAKURUGENZI WAPYA DODOMA

 


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu anawatangazia Wakurugenzi wote wapya 69 walioteuliwa kwa mara ya kwanza, kuripoti  Makao Makuu ya Ofisi za Rais –TAMISEMI – Dodoma tarehe 05.08.2021 kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma – Mkapa House kuanzia saa tatu asubuhi kwa ajili ya kupatiwa maelekezo mbalimbali.

Wakurugenzi hao wanatakiwa kuripoti wakiwa na cheti cha kuzaliwa, Kitambulisho cha Tifa (NIDA),  Wasifu Binafsi (Cv), Vyeti vya Kitaaluma  pamoja na picha mbili (Passport Size).

Wakurugenzi ambao wamehamishwa vituo vya kazi na wale walioendelea kuwepo kwenye vituo vyao vya awali, waendelee na utaratibu wa kwenda kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi kwa ajili ya makabidhiano kuanzia tarehe 03.08.2021

Halkadhalika Wakurugenzi ambao uteuzi wao umesitishwa, wanatakiwa kwenda kuripoti kwa Makatibu Tawala wa Mikoa husika mara moja.

Post a Comment

0 Comments