WORLD VISION YAPONGEZWA KUJALI AFYA ZA WANANCHI KONGWA



📌MWANDISHI WETU

MKUU wa Wilaya ya Kongwa Remedius Mwema amelipongeza shirika  la World Vision Tanzania kwa kuwezesha wananchi  1800 kutoka wilaya hiyo  kupata uhakika wa matibabu baada ya kuwapatia bima ya afya ya CHF iliyoboreshwa.

Akizungumza wakati wa kukabidhi kadi za CHF  zenye thamani ya 9m/= kwa kaya 300 katika kijiji cha Mkoka wilayani Kongwa,DC Mwema ameyataka mashirika mengine kuiga mfano wa World Vision katika kujali afya za wananchi.

Tunazungumzia uchumi,hatuwezi kuwa na uchumi mzuri kama wananchi hawana afya nzuri.Hivyo nawapongeza sana World Vision kwa kujali afya za wananchi kupitia bima ya afya.

DC Mwema pia amewataka viongozi vijiji na kata katika wilaya hiyo kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya afya kwani kufanya hivyo kutasaidia uboreshwaji wa huduma za afya katika maeneo yao.

Mkuu wa Wilaya pia amewataka viongozi hao kuweka ajenda ya bima ya afya katika kila kikao wanachokifanya ili iwe sehemu ya kuhamasisha wananchi ili kufikia asilimia 40 ya kaya zote katika wilaya ya Kongwa.

World Vision wametuonesha mfano,nawapongeza sana kwa hili.Tuendelee kuhamasisha wananchi katika maeneo yetu ili kaya nyingi zaidi wajiunge kwenye mpango huu wa bima ya afya.





Baadhi ya wanufaika wakipokea kadi zao za CHF kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa


Naye mganga mkuu wa wilaya ya Kongwa Dkt.Thomas Mchomvu ameshukuru shirika hilo kwa nia yake ya dhati ya kuboresha afya kwa wananchi wa wilaya hiyo.

Dkt.Thomas amesema awali ambi lililomfikia kutoka shirika hilo ni kuhudumia watoto lakini baada ya majadiliano na watendaji wa shirika hilo walikubali kutoa bima kwa familia nzima ya walengwa.

Niwashukuru kwa ‘flexibility yenu,maana tungemuhudumia mwanafunzi tu mambo bado yangekuwa magumu siku mzazi atakapoumwa,bado huyohuyo mwanafunzi angepata mzigo wa kuuguza hivyo walikubali kuiunganisha kaya yote

Pia ameongeza kwamba maelekezo yaliyopo wilaya Kongwa inatakiwa kufikia 30% kutoka 12% ambayo ni sawa na kaya 7264 zilizojiunga na CHF kati ya kaya 61995 zilizopo wilayani hapao.

Kaimu Mratibu wa Mradi eneo la Kongwa Zacharia Shigukulu akisoma ripoti ya mradi mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kongwa

Baadhi ya wananchi walioudhuria halfa ya kukabidhi kadi za bima ya afya ya CHF


Kwa upande wake Kaimu mratibu wa mpango huo eneo la Kongwa,Zacharia Shigukulu amesema kwamba mpango huo unatekelezwa katika awamu mbili na awamu ya kwanza .

Pia Shigukulu amebainisha kwamba mpango huo unatekelezwa katika vijiji 10 vilivyopo katika kata ya Makawa,Matongoro pamoja na Mkoka ikitarajiwa kuwanufaisha wananchi zaidi 36,621 kutoka kwenye kaya 8027.

Kaimu Mratibu pia amesema malengo ya mradi huo ni kuunga mkono juhudi za serikali za kuboresha afya na ustawi wa watoto na familia zao na maisha ya jamii na katika kaya hizo 300 zilizokabidhiwa kadi zinajumuisha watoto 1200 na watu wazima (wazazi/walezi) 600.



Burudani ya ngoma za asili zilikuwepo pia


Post a Comment

0 Comments