VIJANA WATAKIWA KUTIA NGUVU UJENZI WA NYUMBA ZA IBADA

 



📌JOSEPHINE MTWEVE NA ZAINABU MTOI

VIJANA wametakiwa kutumia nguvu kazi zao  kwa kushiriki katika shughuli za kimaendeleo na kijamii badala ya kukaa vijiweni na kuinyoshea vidole serikali.

Ushauri huo umetolewa na Shekhe wa kata ya Chang’ombe Ibrahimu Kidura alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari  baada ya kushiriki dua na ujenzi wa msikiti wa kisasa wa  Mccadam uliopo katika kata ya Chang’ombe jijini Dodoma.

Shekhe Kidura amewataka vijana kuhakikisha wanatumia nguvu   walizokuanazo kwenye shughuli mbalimbali za kimaendeleo ikiwemo ujenzi wa nyumba za ibada.

Vijana ndiyo wenye nguvu na wanaweza kushiriki kikamilifu shughuli mbalimbali za kimaendelea ikiwemo na ujenzi, hivyo nawaomba vijana wajitokeze kwa wingi pale shughuli hizo zinapojitokeza

Naye Shekhe Hussein Jumbe amewataka waumini wa dini ya kiislamu kata ya Changombe kuonyesha mfano wa kuchangia mali na fedha kwaajili ya ujenzi wa msikiti badala ya kutegemea watu wa nje na eneo hilo.

Shekhe Jumbe amesema waumini wa kata hiyo wana wajibu mkubwa wa kuonyesha mfano katika kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati kutokana na michango yao watakavyojitoa.

Ninawaomba waumini wa kata hii kujitokeza kwa wingi katika kushiriki ujenzi huu wa msikiti ili uweze kukamilika kwa wakati

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Baraza Kuu la Waislamu Wilaya ya Dodoma (BAKWATA) Bashiru Omari amewaomba waumini kutumia nguvu kazi zao ili kupunguza matumizi ya fedha. 

Bashiru amesema kuwa wakitumia nguvu kazi na kujitoa kwa wingi ujenzi huo utaweza kukamilika kwa wakati.

Post a Comment

0 Comments