TAASISI ZA UMMA ZATAKIWA KUZINGATIA SHERIA YA SERIKALI MTANDAO NAMBA 10 YA MWAKA 2019

                                     

📌HAMIDA RAMADHAN

TAASISI za Serikali zimetakiwa kununua Mifumo au miundombinu ya tehama iliyo Salama  na inayoendana na malengo ya Taasisi zao na zimetakiwa zifanye  Uchambuzi   wa kina na zianishe mahitaji  ili waweze kununua mfumo husika .

Akiongea na waandishi wa habari kwenye ofisi za mamlaka mtandao  katika mji wa serikali Mtumba wakati akihitimisha wiki ya ya uelimishaji umma kuhusu Sheria ya serikali mtandao  Jijini hapa  kamishina Msaidizi wa Jeshi la polisi  na Meneja wa huduma za Sheria-  Mamlaka ya Serikali mtandao (EGA) Raphael Rutaihwa amesema mamlaka hiyo lazima isimamimie Taasisi za serikali kununua Mifumo ya tehama inayoendana na mahitaji yao  na itakayoweza kutatua matatizo  ya  Mifumo.

Lazima tuangalie matataizo gani kwenye Taasisi zetu na tunataka kupata tija gani,na tunataka kuwekeza kiasi gani kwa sababu Mifumo ni uwekezaji mkubwa na inachukua kiwango kikubwa cha pesa lazima tujue thamani ya fedha bila kusahau tija kwani tu atakuwa kufahamu tumepata tija gani kulingana na uwekezaji wetu  kwenye Mifumo

Aidha amesema mamlaka imepewa jukumu la kuhakikisha kwamba  inawezesha Taasisi za umma Mifumo iliyojengwa inakuwa Salama na ndio maana imekuwa ikifanya tathimini ya mara kwa mara  kwa kushirikiana na vyombo vingine ili kuhakikisha Mifumo inayotumika serikali ni inakuwa Salama  kwa maana taarifa za serikali haiwezekani kuvuja 

Amesema Usalama la Mifumo ni jukumu la mamlaka  kwa kushirikiana na Taasisi za umma na hiyo imekuwa ikifanyika kwa kuwawezesha wataalamu waliopo katika taasisisi za umma au kuzishauri taasisi za umma  kuwa  uwezo wa mara kwa mara  kwani teknolojia imekuwa ikibadilika kila siku.

 Pia Sheria namba 10 ya wala 2019O ya serikali mtandao inaelekeza Taasisi yoyote ya umma isijenge wala kuendeleza Mradi wowote wa tehama bila kupata Idhini ya mamlaka.

Sheria imeelekeza Taasisi zote za umma chini ya mamlaka zifanye tafiti ya Mifumo itakayoweza kusaidia matatizo ya nchi.

 

Post a Comment

0 Comments