WAZIRI MCHENGERWA AWAKUMBUSHA TAKUKURU KUFUATILIA MIRADI YA MAENDELEO

 


📌RHODA SIMBA

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora Mohamed Mchengerwa amewataka viongozi wa Taasisi ya  Kuzuia na Kupambana na  Rushwa (TAKUKURU) kufatilia vyema  utekelezaji wa miradi yote ya kimaendeleo inayoendelea hapa nchini na wahakikishe kuwa kusiwepo na mianya ya rushwa

Aidha amewaagiza viongozi hao kuongeza jitihada katika kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kujua haki zao na waweze kuepukana na vitendo vya kutoa na kupokea rushwa.

Ameyasema hayo leo octoba 25 jijini hapa wakati akifungua mkutano mkuu wa  mwaka wa viongozi 60 kutoka katika wilaya 28 za kitakukuru, wenye lengo la kujadili utendaji kazi, pamoja na changamoto katika kazi zao.

“Utekelezaji wa miradi ya kiimaendeleo umegubikwa na  udanganyifu ninyi kama TAKUKURU kiongozi wa kila wilaya apimwe namna anavyoweza kusimamia  matumizi ya fedha katika kila wilaya na niseme tu kwamba hili ni  jukumu letu  sotekatika kusimamia kusimamia,

“Mheshimiwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan alivyofungua hizi fursa za uchumi  hakumaanisha watu watumie fedha hizo vibaya  na kutumia nyaraka za uongo kuhusu gharama zinazotumika  katika miradi  hiyo tumieni mkutano huu kujadili malengo na muhakikishe kusiwepo na mianya ya uchepushaji wa fedha hizo kwaajili ya matumizi binafsi katika kila mradi”amesema Mchengerwa.

Aidha amesema Taasisi hiyo isionekane na kasoro ya rushwa  na badala yake iwe mstari wa ,mbele kufanya kazi usiku na mchana ili kuokoa rasilimali za taifa .

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kondoa  Hamis Mkanachi akiongea kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Dodoma Anthon Mtaka amewataka  viongozi hao kutumia mkutano huo kujadili tathimini ya mwaka mzima  na Zaidi wajikite katika kutatua uzembe  pamoja na kutowajibika kwa baadhi ya viongozi wa taasisi hiyo.

Wito wangu kwenu  ni kwamba tathmini yetu iwe ya kina na  tutazame namna tutakavyoweza kujipambanua katika kila wilaya namna bora ya utendaji.

Kwa upande wake  Mkurugenzi Mkuu kutoka katika Taasisi ya kuzuia  na kupambana na rushwa  TAKUKURU  Salumu Hamduni amesema wametekeleza majukumu na kwa kipindi cha mwaka 2020 hadi 2021 jumla  ya shilingi billion 29.3 ziliokolewa ambapo billion 11 .2 ziliokolewa kwa mfumo wa fedha taslim  na utaifishaji mali na kiasi cha  bilioni 18 zilidhibitiwa kabla hazijatumika.



Amesema miradi ya kimaendeleo 1,188 zenye thaman ya billion 714.17 katika sekta ya  afya maji elimu  ziliweza kufatiliwa na kuona makosa  ambayo wameyachukulia hatua.

Tumeelimisha katika ngazi ya makao makuu pamoja na wakuu wa takukuru kuzuia vitendo vya rushwa kuelimisha, kushirikisha jamii pamoja na kuwafikisha watumiwa mahakami kwa kushirikiana na ofisi ya Taifa ya  mashtaka  majalada 1,053 yalichunguzwa na kukamilishwa .

Pia amesema katka majalada hayo,majadala  339 yaliwasilishwa kwa mkurugenzi  wa mashitaka kuomba kibali cha kuwafikisha mahakani ambapo kesi mpya  zilipatikana 542, na kesi 541 zilitolewa uamuzi ambapo Jamhuri iliweza kushinda kesi 345.

Aidha akizungumzia changamoto zinazoikabili Taasisi hiyo Hamduni amesema ni pamoja na ufinyu wa bajeti ambao umeathiri uchunguzi, mafunzo kwa wafanyakazi, ununuzi wa vifaa na mahitaji mbalimbali  pamoja na uhaba wa wafanyakazi

Hata hivyo Mkutano huo wa siku tatu wa viongozi wa TAKUKURU umebebwa na kauli mbiu isemayo  ” kupambana na rushwa ni jukumu lako”

 

Post a Comment

0 Comments