SIMBACHAWENE ATAMANI MAREKEBISHO YA SHERIA YA USIMAMIZI NA UDHIBITI WA SILAHA NA RISASI

 


📌RHODA SIMBA


WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene amesema jumla ya silaha 228, zimesalimishwa kwa Jeshi la Polisi  huku  silaha aina ya gobore imeoneka ikiongoza kwa asilimia 76.3.

Kadhalika ameliagiza jeshi hilo  kuangalia upya uwezekano wa kufanya marekebisho ya Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Silaha na Risasi ya Mwaka 2015.

Ameyasema hayo leo  December 6 jijini hapa  wakati  akizungumza na waandishi wa habari , kuhusu  utekelezaji wa tangazo la msamaha kwa usalimishaji wa silaha haramu lililoanza mnamo  Novemba 1 hadi 30 mwaka 2021

Amesema kufanya hivyo ni  kuweka utaratibu wa kisheria wa kutengeneza  na kuruhusu Magobore kwa kuwa silaha hizo zimekuwa zikitumika kwa shughuli za ulinzi katika jamii.

 Kwa mchanganuo wa PISTOL 05 sawa na 2.2% ya silaha zote zilizosamilishwa, magobore 174 sawa na 76.3% ya silaha zote zilizosalimishwa, S/gun 38 sawa na 16.7% ya silaha zote zilizosalimishwa, Rifle 10 sawa na 4.4% ya silaha zilizosalimishwa   na SMG 01 sawa na 0.4% ya silaha zote zilizosalimishwa

Pia imesalimishwa jumla ya mitutu 12 ambapo mitutu 11 imesalimishwa Mkoa wa  Tanga na Mtutu 01 umesalimishwa  Mkoa wa Mbeya.

Amesema kufuatia matokeo haya ya usalimishaji wa silaha haramu,Waziri Simbachawene amelielekeza  Jeshi la Polisi kuangalia upya uwezekano wa kufanya marekebisho ya Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Silaha na Risasi ya Mwaka 2015 ili kuweka utaratibu wa kisheria wa kutengeneza  na kuruhusu Magobole kwa kuwa silaha hizo zimekuwa zikitumika kwa shughuli za Ulinzi katika jamii.

Pia,kufanya misako kwa kutumia taarifa za kiintelelijensia ili  kuwabaini na  kuwakamata wale wote wanaomiliki silaha kinyume na Sheria na kisha kuwachukulia hatua za kisheria.

 

Post a Comment

0 Comments