SERIKALI KUJA NA MPANGO WA KUANZISHA MASJALA YA HEWA YA UKAA ITOKANAYO NA MISITU KUONGEZA UCHUMI WA NCHI.

 

📌JASMINE SHAMWEPU

SERIKALI ina Mpango wa   kuanzisha masjala ya hewa ya ukaa itokanayo na misitu ili kuchangia uchumi wa nchi.

Hayo yamebainishwa   jijini Hapa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro wakati akishiriki zoezi la Upandaji wa miti katika eneo la Iyumbu ikiwa ni mwendelezo wa maadhimisho ya wiki ya Sera mpya ya Mazingira ya mwaka 2021 inayotarajiwa kuzinduliwa Februari 12,2022 na Makamu wa Rais Dkt.Philiph Mpango.

Dkt.Ndumbaro amesema kuna faida kubwa itokanayo na misitu hivyo mkakati wa serikali ni kuhakikisha misitu inalindwa na kuhamasisha upandaji wa miti zaidi.

Amesema Misitu inachangia pato la taifa asilimia 3.5 inazidi sekta nyingine ambazo watu hawajui ndio maana tunasema Misitu ni Mali watu wanafanya Biashara ya mbao, Biashara ya thamani bila kusahau Misitu ndio chanzo cha Mazingira mazuri tuliokuwa nayo.

Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Andrew Komba   amesema zoezi la kujanikisha Dodoma kwa upandaji miti linaratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Pia amesema Februari 10,2022 Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira itatoa elimu kwa jamii katika soko la Chang’ombe namna nzuri ya urejeshaji wa taka ngumu kwa ajili ya matumizi mengine.

Meneja wakala wa misitu Tanzania [TFS] Prof.Santos Silayo amesema amezungumzia faida ya misitu ni pamoja na kuleta mapinduzi makubwa ya viwanda ambapo zaidi ya viwanda 800 vimeanzishwa.

Ikumbukwe kuwa kabla ya kupitishwa sera mpya ya Mazingira ya Mwaka 2021, sera ya Mazingira iliyokuwa ikitumika ni ya mwaka 1997 ambayo imedumu takribani miaka 25 kabla ya kuhuishwa tangu kuanzishwa kwake.

MWISHO.

Post a Comment

0 Comments