📌RHODA SIMBA.
MKUU wa Mkoa wa Dodoma Anthon Mtaka ameitaka jamii ifundishe watoto kuhusu suala la kutopokea wala kutoa rushwa wakiwa wadogo ili wanapokua wakubwa wajue kuwa kitendo hicho si kizuri kwenye maisha yao.
Mtaka ameyasema hayo jijini hapa wakati akifungua mafunzo kwa walimu walezi wa klabu za wapinga rushwa shuleni yaliyoandaliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambapo amesema endapo watoto wakifundishwa kuwa vitendo hivyo si vizuri wakiwa wadogo watakua katika maadili mema.
Kuna shule ipo Wilaya ya Kondoa siku tumefika pale wameanza na salamu rushwa ni adui wa haki ndipo wanaendelea na salamu nyingine kwahiyo tujitahidi kuwajengea uelewa ili wajue wakiwa wadogo na siku zote samaki mkunje angali mdogoRC Mtaka
Amesema kuwa elimu ya kutopokea na kutotoa rushwa itolewe kama ilivyo elimu ya dini itolewayo na kwa watoto wakiwa wadogo shuleni .
“Wakati wanafunzi wapo shuleni kuna umoja wakiwa pale kila mmoja na dini yake wanakaa kusali sasa kwanini kama ilivyo umoja ule tusiwafundishe watoto kujua kuhusu masuala ya rushwa kuwa ni adui wa haki”amesema Mtaka
Kwa upande wake Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Dodoma Sostenes Kibwengo amesema mafunzo hayo yameandaliwa kwa walimu walezi wa klabu za wapinga rushwa lengo likiwa ni kujadili namna gani klabu ziimarike na kuwa mfano mzuri katika kupambana na rushwa.
Lengo ni kujenga kizazi ambacho kitakuwa na maadili kizazi cha watu ambao ni wazalendo na wanawajibika na wenye maadili mazuri kwa kufanya hivyo sisi tutakuwa hatuna kazi ya kupiga makelele achana na rushwaKibwengo
0 Comments