📌JAMES K. MWANAMYOTO
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama amesema Serikali ya Awamu ya Sita katika kipindi cha mwaka mmoja cha uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kuzingatia maslahi ya Watumishi wa Umma hivyo kujenga morali ya kiutendaji kwa watumishi hao.
Mhe. Jenista
amesema hayo leo jijini Dodoma wakati wa mkutano wake na vyombo vya habari
uliolenga kuuhabarisha umma kuhusu mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita
katika kipindi cha mwaka mmoja cha uongozi wa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan.
Mhe. Jenista amesema katika kipindi cha mwaka mmoja, Serikali imesimamia mageuzi makubwa kwenye Utumishi wa Umma katika kutazama maslahi ya watumishi, ikiwemo suala la upandishaji madaraja ambapo imewapandisha madaraja Watumishi wa Umma 190,781 wenye sifa stahiki na katika zoezi hilo jumla ya shilingi bilioni 39,649,988, 204 zimetumika.
Mhe. Jenista ameongeza kuwa Serikali imelipa madeni ya mishahara ya Watumishi wa Umma 65,394 yenye thamani ya shilingi bilioni 91,087,826,006.34 ambayo walikuwa wakidai kwa muda mrefu.
Sanjali na hilo, Mhe. Jenista amesema, Serikali imetumia
shilingi bilioni 1,330,306,572 kwa ajili ya kuwabadilisha kada na kuwalipa
mishahara Watumishi wa Umma 19,386.
Katika kuboresha huduma kwa wananchi, Mhe. Jenista amesema,
Serikali imeongeza rasilimaliwatu kwa kutoa vibali vya ajira mpya na mbadala12,336
vilivyogharimu jumla ya shilingi bilioni 7,761,869,809.
Aidha,
Mhe. Jenista amesema, Serikali ya Awamu ya Sita imewapunguzia Watumishi wa Umma
asilimia moja (1%) ya makato ya PAYE kutoka asilimia 9 hadi asilimia 8 lengo
likiwa ni kuwapunguzia watumishi mzigo mkubwa wa kodi hivyo kuwaongeza kiwango
cha mshahara kinachobakia (Net salary) kutokana na kupungua kwa kodi ya PAYE.
Hatua
ya Serikali ya Awamu ya Sita kuzingatia maslahi ya Watumishi wa Umma
kumewawezesha Watumishi wa Umma kuwa na morali ya utendaji kazi yenye tija
katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi.
0 Comments