📌RHODA SIMBA
KAMISAA wa Sensa Tanzania bara na Spika wa bunge msatafu Anne Makinda amesema kuwa utekelezaji wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 umeelekeza nguvu katika ngazi ya chini lengo likiwa ni kufanikiwa zaidi kwa kuwa sensa hiyo ndiyo inayotoa dira ya kupanga maendeleo ya nchi.
Ameyasema hayo leo Mei,24,2022 jijini hapa, wakati akifungua mkutano wa Wadau na Mashirika yasiyo ya kiserikali uliyoandaliwa na ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS),ili kujadili namna ya kutoa elimu na kuhamasisha wananchi ambapo amesema kuwa serikali imeweka mkazo kwa sensa hiyo kwa kuimarisha ili iweze kufanikiwa.
Amesema kuwa sensa hiyo itafanikiwa endepo Mashirika na wadau watatilia mkazo katika utoaji elimu na uhamasishaji kwa wananchi ili wawe na uelewa wa kuhesabiwa.
Serikali inaamini kutokana na upana wa mashirika yasiyo ya kiserikali yana uwezo wa kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi. Mashirika haya yamekuwa mstari wa mbele katika kuchangia shughuli za wadau
Naye Mtakwimu Mkuu wa
wa serikalk Dk. Albina chuwa amesema kuwa serikali haiwwzi kupanga maendeleo
bila kuwa na idadi ya inayofahamika.
"Hii ni sensa
ambayo inaenda kutupa hali halisi ya mwelekeo wa maendeleo. Pia sensa ya mwaka
huu inaenda kuungana na ya majengo tutafahamu mazingira ya watu wabaishi
vipi," amesema Dk. Chuwa.
Ameongeza kuwa suala la takwimu ni la ushirikishwaji wa watu wote hivyo ndio maana zaidi ya Mashirika yasiyo ya kiserikali zaidi 7000 yameshirikishwa ili yakatoe elimu kwa wananchi.
Awali Mwenyekiti wa baraza la mashirika hayo Dk. Lilian Badi amesema kuwa ofisi ya takwimu imeelekeza nguvu nyingi katika kutoa elimu pamoja na kushirikisha Umma kuunga mkono katika zoezi la hilo ambalo linatarajiwa kuanza Agosti 23 mwaka huu.
Mwenyekiti huyo ameeleza kuwa nchi ina Asasi zisizo za kiserikali ambazo zinaundwa na makundi mbalimbali ambayo zaidi ya 700 yamesajiliwa na yanafanya kazi.
" Sisi kama mabaraza tupo wajumbe 30 ambao tunawakilisha mashirika haya 733 yasiyo ya kiserikali, " amesema Mwenyekiti huyo.
Ameongeza kuwa wamejipanga kutumia mitandao yote ya kitaifa yote, makundi ya kijamii na mtu mmoja mmoja wanaoguswa na kazi za Mashirika hayo.
0 Comments