TEHAMA KUWA CHACHU YA MAENDELEO YA KIUCHUMI NCHINI


📌SALMA HAROUN & AGNESS PETER

MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya TEHAMA Dkt.Nkundwe Mwasaga amesema kazi kubwa ya TEHAMA ni kuratibu utekelazaji wa sera ya taifa pamoja na kukuza huduma za TEHAMA kwa lengo la kuwafikia wananchi.

Ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma ambapo amesema sehemu ya kukuza huduma hizo inahusisha sekta binafsi zinazofanya shughuli zake kwa kutumia TEHAMA ambazo zinaweza fanywa ndani na nje ya Tanzania.

Dkt.Mwasaga amesema wanaangalia Mikoa imejiandaa vipi katika mabadiliko ya kidigiti ili kuhakikisha shughuli zote za kibiashara na za kijamii zinafanyika katika mitandao ili kukuza mapato ya mikoa na wengine kutengeneza ajira.

Tunahakikisha Tanzania inapambana na nchi zingine kwenye uchumi wa dunia kuhakikisha kwamba uchumi wetu unakua uchumi wa ushindani

Aidha Dkt. Mwasanga ameongeza kuwa lengo kubwa ni kukuza wanataalamu, kampuni ndogondogo, mikoa ili kuhakikisha mikoa inashindana na kuifanya Tanzania iweze kushindana na nchi nyingine kwenye uchumi mkubwa wa kidigiti wa dunia.

Naye Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Gerson Msigwa amewataka vijana kujitokeza katika kuchangamkia fursa za TEHAMA

Amesema tume ya taifa ya TEHAMA imejiandaa vyema katika kuhakikisha Tanzania inakua katika mfumo wa kidigiti ambapo itaweza kurahisisha shughuli za kiuchumi.

 

 

 

Post a Comment

0 Comments