WANANCHI MKOANI NJOMBE WATAKIWA KUJITOKEZA KUHESABIWA AGOSTI 23

 

📌JOSEPHINE MTWEVE

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi wa mkoa wa Njombe kujitokeza kuhesabiwa Agosti 23 mwaka huu kwa lengo la kuisaidia serikali kupanga majukumu yake kutokana na idadi ya watu.

Ameyasema hayo wakati akikagua ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ambapo amesema kuwa kutokana na takwimu ya watu na makazi itaisaidia serikali katika usambazaji wa madawa.

Rais Samia amesema kwa sasa serikali inasambaza madawa katika hospitali mbalimbali nchini na bado hazitoshi kwasababu idadi ya watu imeongezeka kwa asilimia kubwa.

Niwaombe mjitokeze kuhesabiwa kwasababu mambo yote tunayapanga kutokana na idadi ya watu mkijificha kuhesabiwa tutakuwa tunaleta kidogo ambacho hakitawatosha na wewe uliyejificha utakua unatumia cha mwenzio ambaye alihesabiwa.

Nawaomba wote tukahamasishane kwa hali yoyote mtu aliye mzee, mkongwe, mlemavu, mzima miaka yetu wote tukahesabiwe li mtupe fursa serikali yenu ya kujipanga vizuri

Aidha Rais Samia ameongeza kuwa serikali ipo kwa lengo la kuwatumikia wananchi ambapo amesema wanakwenda kujenga barabara kwa kiwango cha rami ama kwa kiwango cha kupitika mwaka mzima.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt.Winifredi Kyambile amesema kukamilika kwa mradi huo kutawezesha kulaza wagonjwa mpaka 400 tofauti na awali.

Dkt.Kyambile amesema kuna majengo mengine yatakayoongezeka kama vile Chuo kwaajili ya kufundisha wataalamu watoa huduma ya afya pia kujenga nyumba kwaajili ya watumishi.

Kukamilika kwa mradi huu kutaimarisha afya ya wananchi wa mkoa wa Njombe na mikoa ya jirani ambapo mwanzo tulikua tunawapeleka wangojwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya

Naye Waziri wa Afya Ummi Mwalimu ametoa rai kwa wananchi wa mkoa wa Njombe kujiunga na Mfuko wa Bima ya Afya ili waweze kupata huduma za afya bila kikwazo.

 

Post a Comment

0 Comments