📌SALMA HAROUN
MAKAMU wa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt Philip Mpango ameitaka Wizara ya Kilimo kufanya kazi na shirika la Taifa la
Bima ili kuhakikisha wakulima hawapati athari zozote katika kilimo dhidi ya
madhara yatokanayo na mbegu zisizo bora.
Hayo ameyasema leo Agosti 1 Jijini Mbeya katika maonyesho
ya sikukuu ya Nanenane wakati akipita katika mabanda ya waliohudhuria maonyesho
hayo. Mpango amesema suala hilo waweze kulifanyia kazi ili wakulima waepukane
na changamoto katika kupata mbegu zisizo bora ambapo huwasababishia wakulima
hasara wakati wa mavuno.
Amesema kuwa shirika la Utafiti la TARI katika kuwa
wabunifu wanatakiwa kufanya utafiti kwenye mazao mbalimbali yatakayoweza
kutumika katika maeneo tofauti kulingana na ardhi iliyopo nchini.
Kuna mbegu zimeenda kwa wakulima Wilaya ya Katavi zimeleta balaaa hazikuzaa wakulima wamesema TARI imetudanganya, turekebishe taasisi ya TARI ili kuleta ubora wa mbegu
Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Mh Husseni Bashe, amesema ameziagiza Halmashauri zote kuwa wakulima waliotakiwa kulipia mbegu hizo wasilipie mwaka huu ili kuweza kuwapunguzia makali ya athari walizo zipata mwaka jana
Amesema wakulima wawe na utayari wa kukabiliana na
changamoto zitokanazo na mabadiliko ya hali ya hewa ambapo pia ni chanzo kimojawapo
cha mazao kutokubali katika maeneo yao.
Wakulima walifundishwa kupanda zao la alizeti wakati mvua zinaendelea kunyesha, wakati wakulima wamepanda hali ya hewa haikuweza kukubali na kupelekea wakulima kuathirika hususani katika nyanda za juu kisini.
0 Comments