ALIYEUWA NA KUTUPA MTOTO MCHANGA AKAMATWA.

 

📌SALMA HAROUN.

JESHI la Polisi limemtia mbaroni Nasra Khalifa mwenye umri wa miaka 24 ambaye anatuhumiwa kwa kosa la kumuuwa na kumtupa mtoto mchanga katika maeneo ya Uhindini Jijini Dodoma anaye kisiwa kuwa na masaa machache duniani.

Akizungumza katika mahojiano maalumu kamanda wa jeshi la polisi, Martini Otieno amesema mtuhumiwa huyo alifika katika Hospitali ya Makole kwa kudai kusumbuliwa na matatizo ya tumbo na kuomba kuelekea chooni ambapo alikaa kwa mda mrefu hali ambayo iIiuwatia hofu wauguzi.

Amesema wauguzi walifanikiwa kumkuta mtuhumiwa huyo akiwa amejifungua mtoto wa kiume na kufanya jitihada za kumtumbukiza katika tundu la choo.

Sababu iliYosababisha mtuhumiwa kufanya hivyo ni kutokuwa na maelewano mazuri kati yake na   mwenzake   hali ambayo imemsababisha kufanya tukio hilo

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtaa huo, Alnoor Kassam ameonesha kusikitishwa na tukio hilo na kukemea vikali watu wanaotenda vitendo hivyo.

Hata kama umeachika kuna utaratibu wake wa kufanya lakini sio kutupa mtoto

Naye Mkazi katika mtaa huo, Muslim Mohammed ameoneshwa kuumizwa huku akiomba serikali kuchukua hatua kali kwa baadhi ya  watu wenye kutenda vitendo hivyo nchini.

Amesema sheria kali zichukuliwe kwa baadhi ya watu wanaotenda vitendo hivyo ili viwe fundisho kwa watu wengine.

Tuendelee kukemea suala hili liishe hata kama mtu ana dhiki za maisha ajue kupambana nazo kuliko kufanya ukatili kama huu

 

 

Post a Comment

0 Comments