📌RHODA SIMBA
AFISA Mtendaji
Mkuu,Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Milton Lupa amesema
kumekuwa na ongezeko la ununuzi kutoka takribani Tani 58,000 kufikia
zaidi ya tani 110,000 za nafaka kwa mwaka 2021/2022.
Pia
ununuzi wa nafaka kwa msimu mwaka2022/2023 unaendelea kupitia Kanda za
Sumbawanga,Songea, Arusha,Shinyanga ,Makambako,Songwe na Dodoma.
Hayo
yamesemwa leo Jijini Dodoma Wakati akitoa taarifa kuhusu utekekezaji wa
majukumu ya NFRA katika Kipindi cha Serikali ya awamu ya sita.
Amesema
ongezeko la hifadhi ya chakula imewezesha wakala kuwa na akiba ya
kutosha ya chakula kwa ajili ya kuhudumia kwa wakati mahitaji mbalimbali
ya dharura au Upungufu wa chakula unaoweza kujitokeza nchini.
Serikali ya Rais Samia imeimarisha Hifadhi ya Chakula Nchini kwa kuongeza akiba ya chakula inayohifadhiwa na wakala kuwa zaidi ya mara mbili ya kiasi kilichokuwa kinahifadhi kipindi cha miaka mitatu ya hivi karibuni
Na
kuongeza "Wakala umepata mafanikio makubwa katika Serikali ya awamu ya 6
inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu
Hassan ambayo imekuwa ni nguzo imara ya kuongeza ufanisi wa NFRA katika
utekelezaji wa majukumu yake," Amesema Afisa Mtendaji huyo Lupa
Aidha
amesema kuwa Serikali ya awamu ya 6 imewezesha NFRA kuimarisha uchumi
wa makundi mbalimbali yakiweno ya wakulima,vyama vya ushiriki,sekta
binafsi na wananchi kwa ujumla kupitia mapato yanayopatikana kwa kuuza
nafaka kwa NFRA hivyo kuwa na soko la uhakika kwa wakulima.
Ameeleza
wakala umekuwa ukinunua nafaka kwa bei nzuri hivyo kuwa soko tegemezi
kwa wakulima wengi na kuwapa motisha wakulima kujishughulisha na Kilimo.
Jukumu
kuu la NFRA ni kuihakikisha Nchi usalama wa chakula kwa kununua na
kuhifadhi akiba ya chakula na kutoa chakula Cha msaada kwa waathirika
waliokubwa na majanga mbalimbali ya kitaifa,Aidha wakala huzungusha
akiba ya chakula kwa lengo la kutoa la nafasi ya uhifadhi na kuingiza
mapato ya kununua akiba mpya ya chakula,Mazao yanayonunuliwa na
kuhifadhiwa kwa sasa ni mahindi,mtama na mpunga.
0 Comments