WATANZANIA WAHIMIZWA KUJISOMEA VITABU

📌PASCHAL NKWABI

Watanzania wametakiwa kuchagua na kujisomea vitabu vyenye maudhui yanayokuza maarifa ili kuondokana na vikwazo vya umaskini na ujinga sanjari na kutumia maarifa  hayo kuleta mabadiliko miongoni mwa jamii

Rai hiyo imetolewa leo Jijini Dodoma kwenye uzinduzi wa kitabu cha ukombozi kutoka kitabuni chenye maudhui ya dini na maisha ya kwaida.

Mstahiki Meya wa Halmashuri ya Jiji la Dodoma Prof: Device Mwamfupe kwa niaba ya Naibu Waziri Wizara ya Kilimo Anthony Mavunde ambapo mara baada ya uzinduzi huo amesema itakuwa na manufaa kwa watoto hasa kumtambua Mungu.

Amesema kuwa uzinduzi wa vitabu si kitendo cha kukata utepe pekee kuashiria tendo husika, lakini uzinduzi halisi ni ile hali ya kukipata kitabu chenyewe kukisoma na kutumia maarifa yaliomo kwenye kitabu hicho kwa lengo la kujiletea mabadiliko chanya kwenye maisha.

Profesa Mwanfupe ameeleza kuwa  binadamu ana minyororo mingi ikiwemo ya ujinga, kutawaliwa na watu wengine  na dhambi, hata hivyo amesema kuwa mnyororo  mkubwa ni wa kutofahamu au kuwa mjinga akitoa mfano wa mtu kukasirika na kujinyonga kwenye tawi la mpampai kuonesha hali ya kutojua hata namna  mjinga asiyeweza  kuamua hata kwenye uamuzi wa kijinga.

Amesema kuwa minyororo hiyo inaweza kufunguliwa kwa kutumia maarifa hasa ya kujisomea  akitumia muktadha wa uzinduzi wa kitabu hicho  kuwa Mungu ni chanzo cha kiu ya kuondokana na minyororo hiyo.

Kuhusu kusoma amewataka wazazi kuchagua vitabu vizuri vinavyoweza kuwafanya watoto wao kuongeza maarifa zaidi ikiwemo kuchagua vipindi vya Runinga pamoja na sinema zenye kukuza ujuzi chanya na sio za mauaji au mapigano. 

Amewakumbusha watanzania kutonunua vitabu na kuviweka maktaba kwenye nyumba zao kwa mkumbo akimanisha kutozitumia kujisomea au kusoma vitabu wanavyonunua akiwataka kuzitumia maktaba hizo kusoma.

Bwana Maneno Mung’ong’o ambaye ni mtunzi na mwandishi wa kitabu hicho amesema kuwa ameandika na kuzindua kitabu hicho ili kuamsha ari ya usomaji, ununuzi na utunzaji wa vitabu, utamaduni unaoonekana kutoweka kila uchwapo hapa nchini.

Kwenye maelezo yake bwana Mugo’ng’o amesema kuwa katika uzoefu wake amegundua kuwa, wasomaji wa vitabu ni wachache, licha ya mabadilko ya uboreshaji wa nyumba  nyingi hazina maktaba ,na wazazi kutowaononesha watoto wao ari ya kujisomea vitabu.

Ameonya kuwa hali hiyo ni hatari hasa kwenye dunia hii ya ushindani yenye  ukosefu wa ajira ambayo inataka jamii isome vitabu vya kutosha kuongeza maarifa ili kukuza ujuzi wa kupambana na mzingira pamoja na kuleta maendeleo chanya.

Ameshauri wazazi na shule kukuza mifumo ya utunzaji wa vitabu kwa lengo la kusomwa na wanzafunzi akisema, itasaidia kizazi cha sasa kupenda kujisomea, yeye binafsi akiahidi kuanzisha klabu za usomaji wa vitabu

Miongoni mwa watu walioalikwa na kuhudhuria uzinduzi huo ni Bwana Francis Mlelwa alipozungumzia juu kitabu hicho amesema  baada ya kusoma kitabu hicho amegundua kuwa kuna mambo mengine mtu anaweza kutojua asiposoma lakini akisoma huenda anaweza kujua mengi zaidi .

Uandishi na   vitabu bado ni utumaduni muhimu sana kwenye kuongeza maarifa ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla hasa unapotumika kuleta mabadiliko chanya miongoni mwa jamii.

 

Post a Comment

0 Comments