UNFPA IMEAHIDI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI YA TANZANIA

 ðŸ“ŒRHODA SIMBA

SHIRIKA la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya Watu Duniani (UNFPA) limeahidi kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kutoa elimu na kuhakikisha wananchi wanatambua matumizi sahihi ya matokeo ya Sensa ya watu na makazi iliyofanyika Agosti 23 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma mara baada ya kufanya mazungumzo na mwakilishi mkazi wa UNFPA Wilfred Ochuan ambaye anamaliza muda wake hapa nchini, Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi Anne Makinda amesema matokeo ya Sensa yanatakiwa yalete tija kwa wananchi katika kufikishiwa shughuli za maendeleo na huduma za kijamii.

Katika shirika lililotusaidia sana kufanikisha sensa yetu hii ni UNFPA kwasababu kimataifa wao ndio wanao simamia mambo ya idadi ya watu

Makinda.

Amesema walikuwa wanasaidia kwenye mambo ya ufundi, vifaa na kuwashirikisha na mataifa mengine ikiwemo kupata vishikwambi 600 kutoka South Korea, 200 kutoka UN WOMEN na China.

Huyu Wilfred Ochuan ameteuliwa kwenda Ghana kuwa mwakilishi wa idadi ya watu hivyo alikuja kutuaga na kuaga wafanyakazi wa hapa

 Makinda.

Yeye ameahidi kwamba wataendelea kutusaidia ili watu waweze kujua matumizi ya takwimu sasa hatuna mila sana ya kutumia takwimu lakini kwa sasa tunataka hilo liweze kuonekana kabisa

Pia amesema watatumia takwimu hizo kufanya mipango yao, ufatiliaji wa maendeleo mbalimbali ili ziweze kutumika kwenye bajeti ya serikali na waliahidi Euro laki 2.

Tujaribu kutafuta mbinu zote watanzania tuanze kutumia hizi sensa, kwani sensa zinagharama sana kwahiyo huwezi kufanya kitu kwa gharama halafu badae unakiacha tu

Kwa upande wake Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt Albina Chuwa amesema Tanzania ina watu wakarimu kama ilivyo kwa wananchi wa nchi ya Ghana ambao nao pia siku zote wameonekana wakarimu hivyo tuna imani utakwenda kutusaidia kupeleka picha ya nchi ya Tanzania ilivyo .

Bila shaka tunaimani utachukua yale yote mazuri yaliyopo Tanzania kwani hata Rais wetu wa awamu ya sita Samia Suluhu Hassan amekuwa akiishangaza dunia  kwa mambo makubwa anayoendelea kuyafanya

Chuwa amesema katika suala zima la takwimu nchi ya Tanzania imekuwa bingwa na imeonekana ni nchi inayoendelea kukua kiuchumi kwa takwimu za Afrika  .

Mafanikio hayo yote yamekuja kutokana na kuwa na mawasiliano na uwazi kwani ndio kitu kikubwa kwetu na pia tunajivunia kuwa na mtu kama mama Anna Makinda ambaye ndio aliyekuwa kamisaa wa sensa Tanzania bara

Akizungumza Naibu Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa UNFPA anayemaliza muda wake Wilfred Ochang   aliishukuru serikali kwa kuweza kushiriki katika zoezi zima la sensa kwani ameweza kujifunza mambo mengi mazuri na makubwa juu ya masuala yote ya sensa.

 Nawahakikishia kuwa naenda kupeleka mazuri yote yaliyomo na niliyoyapata katika nchi ya Tanzania, na hongereni kwa kuweza kufanikisha zoezi zima la sensa ya watu na makazi

Kwa nchi ya Ghana tunakwenda kufanya sensa ya kidigitali mwezi mei 2023 japokuwa tumechelewa lakini tunaendelea kujifunza na hakika nitakwenda kupata uhakiki baada ya kukamilika kwa zoezi zima la sensa  ya kidigitali hivyo naomba ushirikiano kutoka kwenu



 

 

Post a Comment

0 Comments