📌MWANDISHI WETU
MKUU
wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amekabidhiwa vyumba 14 vya madarasa na
ofisi 9 za walimu zilizokamilika kwa fedha zilizotolewa na Serikali kwaajili ya
ujenzi wa vyumba vya madarasa ili wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023
waweze kupata madarasa ya kutosha ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Bahi.
Halmashauri
ya Wilaya ya Bahi ikiwa ni miongoni mwa Halmashauri 8 za mkoa wa Dodoma zilizopewa
fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa ilipokea shilingi Milioni 280 tarehe 8
Oktoba, 2022 na imeweza kuwa Halmashauri ya kwanza kukamilisha ujenzi wa vyumba
hivyo na kukabidhi tarehe 12 Disemba, 2022 huku kila darasa likiwa na viti 40.
Akisoma
taarifa ya ujenzi huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Bwana Athumani
Masasi amesema kuwa
Vyumba vya madarasa 14 na ofisi 9 vimejengwa katika shule zote 8 za Halmashauri ya Wilaya ya Bahi ikiwemo shule ya sekondari ya Bahi iliyokabidhi vyumba 5 na ofisi 2, Idihwa darasa 1 na ofisi 1, Kigwema madarasa 2 na ofisi 1, Chikola darasa1 na ofisi 1, Chipanga darasa 1 na ofisi 1, Chibelela darasa 1 na ofisi 1, Msisi Juuma madarasa 2 na ofisi 1 na Lamaiti darasa1 na ofisi 1.
Aidha
Mhe. Senyamule ametoa pongezi kwa Halmashauri hiyo na kutaka iwe ya mfano kwa Halmashauri
nyingine zilizopo ndani ya Mkoa na kusema;
Mhe Rais wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ana nia ya dhati ya kutaka kuondoa ujinga kwa kuimarisha sekta ya Elimu ambapo ametoa fedha za kuongeza vyumba vya madarasa 8,000 nchi nzim ambapo kwa Mkoa wa Dodoma tumepata jumla ya vyumba vya madarasa 339
Senyamule
Hata hivyo RC Senyamule ameongeza kuwa Mhe. Rais ametekeleza miradi ya maendeleo kwa zaidi ya asilimia 80 kwa Mkoa wa Dodoma huku vituo vya afya, zahanati, madarasa na huduma zingine zikizidi kuimarishwa.
0 Comments