RAIS SAMIA AKABIDHIWA TUZO YA KIMATAIFA YA INTERNATIONAL ICONIC AWARDS

📌MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Dkt. Pindi Chana amepokea tuzo ya Kimataifa International Iconic Awards ya nchini India iliyotolewa kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan .

Tuzo hiyo imekabidhiwa Disemba 11,2022 Jijini Dodoma na Uongozi wa Miss Jungle International na Bega kwa Bega na Mama (BBMF) .

Kutolewa kwa tuzo hiyo kwa Rais  kunatokana na  Programu ya Tanzania – The Royal Tour  aliyoifanya  iliyoitambulisha nchi kitaifa na kimataifa kutokana na vivutio  vya utalii vilivyopo Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar ambayo imesaidia kuvutia watalii wengi.



Post a Comment

0 Comments