JKT YATOA UFAFANUZI KUHUSU VIJANA 147 WENYE MAAMBUKIZI YA VVU

 


 ðŸ“ŒJASMINE SHAMWEPU

 JESHI la kujenga taifa(JKT) limeelezwa kusikitishwa na habari iliyotolewa kwenye baadhi ya vyombo vya habari hivi Karibuni la vijana wa JKT 147 kuwa na maambukizi ya VVU.

Aidha jeshi hilo limevitaka vyombo vya habari na mitandao ya kijamii vilivyoripoti habari hiyo kwa kuweka picha za vijana wa JKT ambao siyo wahusika wa habari hiyo,kuomba rambi na kuondoka picha hiyo mara moja.

 Akitoa ufafanuzi  huo Mkuu wa tawi la utawala JKT Brigedia General Hassan Mabena amesema kuhusiana na taarifa hiyo vijana wa kundi la lazima (wahitimu wa kidato Cha sita)huendeshwa Kwa kipindi Cha miezi mitatu.

"Kabla ya kuanzia mafunzo vijana hufanyiwa usaili wa nyaraka zao pamoja na vipimo vya afya ili kufahamu utimamu wa mwili"amesema Mabena

Mabena amesema vijana ambao majibu ya vipimo vyao huwa na changamoto za kiafya hufanya mafunzo yao chini ya uangalizi wa wakufunzi ili kuhakikisha wanamalizia mafunzo yao salama.

"Kwa kuwa Hilo ni kundi la lazima,vijana wenye ulemavu wa kuonekana Kwa macho hupokelewa Katika kikosi Cha Ruvu JKT ambacho kina miundombinu ya kuhudumia watu wa jamii hiyo.

 

Kadhalika amesema JKT inasisisitiza kuwa kigezo Cha afya Cha vijana hao wa kundi la lazima wanakuja makambini wakiwa na changamoto za kiafya kinazingatiwa Kwa kuwaweka chini ya ulinzi.

 

Aidha amesema JKT inazingatia sheria kanuni na taratibu za kitabibu sambamba na kuzingatia Mila na desturi za Nchi yetu Katika kutekeleza jukumu lake la msingi la malezi ya vijana.

 

"JKT linapenda kutarifu uma kuwa mafunzo ya JKT ni salama yenye kuzingatia sheria na taratibu za miongozo ya malezi ya vijana wanaopokelewa makambini wanalelewa vizuri kulingana na Mila na desturi za Nchi yetu.

 

Post a Comment

0 Comments