WCF YAPUNGUZA KODI YA MALIMBIKIZO YA MADENI

 ðŸ“ŒRAHMA HAJIA & GETRUDE VANGAYENA

MFUKO  Wa  Fidia Kwa Wafanyakazi(WCF)  wapunguza kiwango  cha kodi ya malimbikizo ya madeni  ya michango ya nyuma kutoka asilimia(10%) hadi kufikia asilimia (2%) ili kuhamasisha waajiri ambao hawajasajiliwa waweze kujisajili na watekeleze wajibu wao wa kulipa michango kwa ajili ya kulinda wafanyakazi wao dhidi ya majanga yatokanayo na kazi

Akizungumza na wanahabari leo jijini Dodoma Mkurugenzi Mkuu  wa  Mfuko Wa  Fidia kwa Wafanyakazi Dkt  John  Mduma  katika mkutano wake wa kueleza utekelezaji wa majukumu ya mfuko  huo katika kipindi cha serikali ya awamu ya sita, amesema WCF imetekeleza sera ya msamaha wa riba kwa waajiri waliochelewesha mchango tangu mfuko ulipoanza ili kuondoa mzigo kwa  waajiri ambao hawakuweza kulipia wafanyakazi wao kwa sababu mbalimbali.

Limbikizo la riba limefutwa kwa wanachama wa mfuko huo na kuwabakizia kulipa Deni msingi tu ambalo ni principal kwenye  mfuko,

Mduma.

Mbali na hayo pia mfuko unajishughulisha kulipa fidia stahiki kwa wakati  kwa wafanyakazi wanaoumia, kuugua na kufariki kutokana na kazi, ambapo hadi kufikia mwaka 2021/2022 umelipa fidia kwa wanufaika takribani  1600 na kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 9.33 kililipwa.

Pia mfuko umeweza kuendeleza kasi ya ujenzi wa viwanda vidogo na vya kati hasa vinavyosindika mazao  ambapo mfuko umefufua mradi wa kiwanda cha chai cha mponde ambapo uzalishaji wake umeanza mwezi Oktoba 2022

Hata hivyo mfuko umeimarisha ushirikiano wa kimkakati na wadau wengine kama  Mfuko wa Bima Ya Afya(NHIF) na hospitali mbalimbali ikiwemo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Taasisi ya Mifupa (MOI), Hospitali ya Benjamini Mkapa na hospitali zingine zote za mikoa  na za Rufaa nchini.

 

Post a Comment

0 Comments