MPANGO AWAPA JUKUMU NEMC KILELE MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

📌WILSON JOHN

MAKAMU wa Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. Philipo Isdor Mpango ametoa maagizo matano kwa Baraza la taifa la kusimamia mazingira pamoja na mamlaka za serikali za mitaa kote nchini kusimamia na kuongeza nguvu katika katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki kama vifaa vya kufungashia bidhaa

Kauli hiyo ameitoa leo Juni 6 katika mkutano wake na wafanyabiashara wa soko la Machinga Complex Jijini Dodoma wakati wa kilele cha maadhimisho siku ya mazingira Duniani iliyobebwa na kauli mbiu isemayo ' Pinga uchafuzi wa mazingira unaotokana na taka za plastiki'

Amesema kumekua na ukiukwaji wa Sheria ambao unafanywa na baadhi ya wafanyabiashara wanaoingiza kinyemela kutoka mataifa ya nje jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo yaliyofikiwa na serikali  ilipotoa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki

Naziagiza Halimashauri zote nchini kusimamia Sheria ndogondogo walizozitunga kuhusu usafi wa mazingira na kuhakikisha mnawachukulia hatua wale wote watakao kiuka maagizo mliyo yaweka,

Lakini pia NEMC mzingatie kampuni zinazopewa majukumu ya kukusanya taka ziwe na utaratibu maalumu wa taka, kwahiyo ninazikumbusha Halimashauri kuacha kutoa tenda kwa kampuni zisizo na uwezo

 Mpango

Hata hivyo Makamu wa Rais amezitaka kampuni na wamiliki wa magari kuwa na sehemu ya kuwekea taka katika gari  ili kupunguza usumbufu kwa abiria na utupaji wa taka ovyo pamoja na  wazalishaji wa taka za plastiki kuhakikisha taka zinazozalishwa zinakusanywa na kuondolewa.

Ni vizuri kila Kaya kuwa na sehemu ya kuhifadhi na kuchoma taka lakini pia wamiliki wa magari wekeni mazingira ya kuhifadhi taka ili kuepusha utupaji wa taka barabarani

Natoa wito kwa sekta binafsi kuongeza jitihada na juhudi ya kukusanya taka kwani taka zinaweza kuwa malighafi na kutumika kama bidhaa zingine, naiagiza Ofisi ya Mh, Suleiman Jafo mtafute  wawekezaji kwa ajili ya hizi malighafi

Mpango

Kwa upande wake Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi, Muungano na Mazingira Mh, Suleiman Said Jafo amesema Ofisi yake kwa kushirikiana na Baraza la taifa la usimamizi wa mazingira (NEMC)  wanahakikisha swala la usafi wa mazingira linasimamiwa vizuri nchi nzima.

Mwaka huu tunataka kufanya tofauti kidogo twende kuleta shughuli za mazingira viwanjani zoezi hili lilianza katika uwanja wa shule ya Sekondari kiwanja cha ndege tulifanya kazi kubwa ya usafi wa mazingira

Na leo Mhe. Makamu wa Rais umefanya kazi kubwa ya kuwaongoza wafanyabiashara wa soko la Machinga Complex kufanya usafi hapa nataka nikuhakikishie kiongozi wa mbio za mwenge nchini Bw, Abdala Shaibu Kaim anasimamia kikamilifu suaala la usafi katika maeneo mbalimbali ikiwemo kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki

Jafo 


 

Post a Comment

0 Comments