WALIOSHIRIKI MASHINDANO YA CECAFA NI WACHEZAJI HALALI WA JKT QUEENS

 ðŸ“ŒSUZANA  ALEX

MSEMAJI wa Timu ya wanawake  JKT QUEENS Masau Bwire amesema  wachezaji  wote walioshiriki  katika mashindano  ya CECAFA   na  mashindano  ya  ndani  ni wachezaji  halali wa JKT  QUEENS ambao wamesajiliwa kwa  usajili  unaotambulika  na TFF mpaka CAF.

Bwire ameyasema  hayo alipozungumza  na CPC BLOG Jijini Dodoma na kubainisha kuwa  mchezaji  yeyote anayechezea timu fulani  huyo ana usajili uliokamilika tayari.

Wachezaji  wote  ambao  tumewatumia katika  mashindano  yote tuliyocheza  ni wachezaji halali wenye usajili   unaokubalika  uwe wa mkopo wa muda mrefu bado  ni  usajiri  unaotambulika  ndio  maana wakacheza kama  kusingekua  na usajiri  wachezaji   hawa  wasingepata  fursa ya kucheza 

Bwire.

Pia  ameongeza  kwa  kusema  wanataka  waonyeshe  kupitia  timu  yao  ya wanawake  watanzania  wanaweza  kufanya  vizuri  kwani timu hiyo  haina wachezaji  wa  nchi za  nje  na badala yake wote  ni wazawa  na hivyo  wameweza  kushinda  ligi  kuu  ya  wanawake   Tanzania.

Sasa tunataka  tuonyeshe  na   huku  upande  wa  wanaume  wapo  watanzania  wenye  uwezo  wana vipaji  na  kila  sababu  ya  kucheza  na  kupata  mafanikio  makubwa  na  tukiwathamini  wachezaji  na  kuwapa  maslahi  yanayoridhisha  kama ambavyo  tumekuWa  tukifanya  kwa wachezaji  wa  nje  hivyo  wanaweza kufanya jambo  kubwa
  

Post a Comment

0 Comments