KISWAHILI NAMBA SABA DUNIANI: TANZANIA YAFUNGUA VITUO 17 NJE YA NCHI KUKUZA NA KUIENEZA LUGHA

 

      



   ðŸ“ŒBAHATI MSANJILA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi amesema lugha ya Kiswahili kutoka Tanzania imeendelea kukua na sasa imefikia kuwa lugha ya saba duniani, huku Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) likifungua vituo 17 katika mataifa mbalimbali duniani ili kuendelea kukuza lugha hiyo.

Prof. Kabudi ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati wakati akizungumza kuhusu mafanikio ya wizara hiyo katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan na kubainisha kuwa ndani ya nchi tayari vimeanzishwa vituo 30 vinavyofundisha lugha ya Kiswahili.

Kwaupande wa Sekta ya michezo amesema Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 161. 977  kwaajili ya ujenzi na ukarabati wa viwanja vya  mashindano ya  mpira wa miguu kwa mataifa ya Afrika (AFCON) yanayotarajiwa kufanyika mwaka 2027.

Akizungumzia Kuhusu  kuziwezesha timu za taifa kufuzu na kushirki  mashindano ya kimataifa  waziri Prof.Kabudi  amesema Serikali imetenga kiasi cha  shilingi Bilion 8.5 

Akizungumza jijini Dodoma, Prof. Kabudi amesema mafanikio hayo ni uthibitisho wa dhamira ya kweli ya Serikali ya kuwekeza katika maendeleo ya vijana, kukuza vipaji, na kuitangaza Tanzania kitaifa na kimataifa kupitia michezo, sanaa, utamaduni na lugha ya Kiswahili. 

Akieleza kuhusu sekta ya utamaduni, Waziri Kabudi amesema Serikali imefanikiwa kuandaa matamasha matatu ya kitaifa ya utamaduni na kuendelea kusherehekea Siku ya Kiswahili Duniani kila Julai 7, baada ya Kiswahili kutambuliwa na Umoja wa Mataifa mwaka 2024.

Prof. Kabudi amesema kuwa mafanikio mengine ni kuanzishwa kwa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari mnamo Machi 3, 2025, hatua inayolenga kudhibiti ubora wa kazi za habari, kuongeza weledi na kuimarisha maadili ya taaluma ya uandishi wa habari nchini.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamagamba Kabudi, ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa mafanikio makubwa katika sekta ya habari, utamaduni, sanaa na michezo ndani ya kipindi cha miaka minne ya serikali ya awamu ya sita.

 

Post a Comment

0 Comments