DC MAGANGA ATOA RAI KWA SHIRIKA LA ELIMU YA AMANI TANZANIA KUTOA ELIMU YA AMANI KWA UADILIFU




📌NA.FAUSTINE GIMU GALAFONI

MKUU wa Wilaya ya Dodoma Mwalimu Josephat Maganga  ametoa rai kwa  shirika  la elimu ya Amani  Tanzania  kuendelea kutoa elimu ya  maadili na amani kwa watanzania ili kuwajengea uwezo wa uzalendo na kulipenda taifa  lao.

Rai hiyo ameitoa jijini Dodoma katika hafla fupi ya kongamano la  shirika la Amani Tanzania hafla ambayo imekutanisha viongozi mbalimbali wa shirika hilo linalojihusisha na kutoa elimu ya amani  hapa nchi tanzania ambapo mkuu huyo wa wilaya amesema  serikali inatarajia mambo makubwa kutoka kwa shirika hilo .

Mmepewa jukumu kubwa katika zoezi la utoaji wa elimu ya  mpiga kura  pamoja na elimu ya amani kwa Taifa letu ,yapo mambo  mengi ambayo tunatarajia kwenu hususan matarajio makubwa kutoka tume ya taifa ya uchaguzi  hasa maadili yaliyosahihi kuelekea uchagui mkuu Oktoba 28,2020.

Mnapopeleka elimu ya maadili mpeleke kwa uadilifu mkubwa ,sisi kama serikali tuna matarajio makubwa kutoka kwenu hivyo muwafikishie walengwa elimu ya maadili kwani ninyi ni mabalozi wa tume ya taifa ya uchaguzi”amesema.

Nao baadhi ya viongozi wa shirika la  elimu ya amani Tanzania akiwemo  rais wa  shirika hilo,Wilson George ,naibu katibu mkuu taifa Zailea Gogo,katibu mkuu elimu ya amani Zanzibar  Ally Saleh Ally  na mwenyekiti wa kongamano hilo Alex Kishimba wameelezea miongoni mwa malengo ya shirika hilo kuwa ni pamoja na kutoa elimu ya amani hapa nchini .


Rais wa shirika la Elimu ya Amani Tanzania,willson George Muunguza kulia akiwa na katibu mkuu Elimu Amani Zanzibar   Ally Saleh Ally .


Shirika la elimu ya Amani Tanzania lilianzishwa rasmi mwaka 2017  kutoka kibali cha wizara ya mambo ya ndani na mwaka 2019 lilipata usajili kutoka wizara ya afya maendeleo ya jamii,jinsia ,wazee na watoto na mwaka huu 2020  ni asasi pekee ya  kiraia iliyopewakibali na serikali kupitia tume ya taifa ya uchaguzi kutoa elimu ya mpiga kura  nchi nzima.



Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mwalimu Josephat Maganga  akiwa upande wa kulia akifuatiwa na Naibu katibu Mkuu Taifa ,Shirika la Elimu ya Amani  Bi.Zailea Gogo.




 
Mwenyekiti wa Kongamano mwaka 2020 Shirika la Elimu ya Amani Tanzania  Alex William Kishimba.

Post a Comment

0 Comments