KANISA LAFUNGA SIKU 21 KUOMBEA AMANI UCHAGUZI MKUU





📌NA HAMIDA RAMADHANI

JAMII imeaswa kuendelea  kudumisha amani na mshikamo na kuachana na mihemko ya kisiasa katika kipindi hiki cha kuelekea mchakato wa uchaguzi mihemuko ambayo itasababisha machafuko hapa nchini na wananchi wachague viongozi wenye Sera zenye tija kwa jamii.

 Akizungumza   katika ibada ya Jumapili Askofu kiongozi wa kanisa la International Evangelism Church lilipo Swaswa mkoani Dodoma  Mchungaji Thadey Silvester amesema wao kama  kanisa liliingia katika mfungo wa siku 21 kwaajili ya kuliombea taifa  katika mchakato wa uchaguzi.

Sisi kama kanisa tumeingia katika maombi ya siku 21 kwaajili ya kuweza kuliombea taifa   tumeona katika kipindi cha uchaguzi kumekuwa na  vurugu vitisho sisi tumeingia katika mfungo huu  wa siku 21 kuendelea kupambana  na hizi roho chafu 
Askofu Thadey

 "Nichukue tu fursa hii kusema kwamba watumishi wa Mungu wawapo madhabahuni watumie muda huu kuhubiri amani na si kufanya siasa katika mahubiri lakini pia hatumzuii mtu kuwa mwana siasa isipokuwa achague moja asichanganye vitu viwili kwa pamoja kama tunavyoona kama Mchungaji Gwajima kajitokeza,kugombea lakini  pia tulikua na marehemu mama Lwakatare, na kuna Mchungaji Msigwa"amesema Mchungaji Thadey

Aidha kwa upande wake Askofu Dr Israel Gabliel Maasa kutoka Arusha amewataka wananchi hasa katika kipindi hiki cha mchakato wa uchaguzi wawachague viongozi ambao watayaenzi mambo yaliyoachwa na  viongozi wengine

Niwaambie tu ndugu zangu tuangalie  na tuchague wale viongozi ambao wanajali watu, wanyonge na watakaotetea maslahi ya wananchi
Askofu Dr Israel Gabliel Maasa 


WITO KAWA VIONGOZI WA DINI

Aidha Askofu Dkt Maasa ametoa wito kwa viongozi wote wakiroho pindi wanapokuwa madhabahuni wasichanyanye siasa na dini.

" Hili nitatizo kubwa sana kiongozi wa dini hatakiwi kuchukua mambo ya siasa na kuyaleta katika madhabahu  hili halifai,"amesema Askofu huyo.

Hata hivyo ameihamasisha jamii na waamini wote wa dini zote waangalie na wachague viongozi ambao wanaleta sera nzuri na si lugha za matusi.

Post a Comment

0 Comments