WWANDISHI WAASWA KUTOANDIKA WAGOMBEA WENYE LUGHA ZA KEJELI



📌NA HAMIDA RAMADHANI

KATIKA kuelekea uchaguzi mkuu  nchini waandishi wa habari wameaswa kuandika na kuripoti habari zenye haki na ukweli na kuachana na wale wagombea wanaojinadi kwa Lugha za kejeli na matusi kwenye mikutano

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Deodatus Balile wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa kufuatia kauli ya aliyekuwa Mbunge wa Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa kuwahamasisha wananchi kuwasusa waandishi wa habari  na kuwataka watumie simu janja ili kupata taarifa za habari.

Tumeona tulisemee hili mapema kwani wakianza kutoa kauli zao hizi ni hatari hasa pale  mwanahabari anapokuwa kwenye majukumu yake hivyo ni lazima tulikemee kwa nguvu zetu zote ili tuwe salama kuepusha vipigo kwa waandishi wetu.Balile.

Na kuongeza kusema kuwa "kwanza  sisi hatuogopi kususiwa na kauli yake ya kusema wametususa atambue kwqmba waandishi wa habari haitutishi bali sisi hatutaandika  habari za mgombea anaetoa lugha chafu ,matusi jukwaani ," amesema Balile

Amesema kwamba kauli yake kwa wananchi ya kusema wawapigwe kidogo hiyo inahamasisha vurugu na kuwachonganisha waandishi na wananchi .

Tumeona katika uchaguzi wa mwaka 2015 waandishi walipigwa Tarime sisi hatupo kwaajili ya kuandika lugha  za namna hiyo isipokua chama cha siasa kijinadi kwa sera nzuri ambazo zina tija kwa jamii
Balile

Aidha amesema kuanzia sasa mgombea yoyote ataye ripoti lugha za matusi  hataripotiwa na kazi ya mwandishi si kuripoti matusi bali ni kuangalia sera zenye tija kwa jamii kama vile Elimu, Afya  na huduma zingine  muhimu kwa wananchi.

"Hivi kuna mtu ambae yupo dunia nyingine jamani hapa wote tunapambana na hawa adui watatu ambao ni Ujinga,maradhi na umasikini" amesema Balile

Hata hivyo amesema nchi za nje ambazo  zimeendelea, ni kutokana na wagombea wao kuwa na  Sera zenye tija na sio Sera za matusi.

VYAMA VYA SIASA.

Aidha amesema vyama vya siasa vihakikishe vinatoa taarifa kwa vyombo vya habari kwani wana habari si wanasiasa na kila mgombea anataka kuonekana.

Ni kweli hatuwezi kuwepo kwenye kila matukio,jambo kubwa na la muhimu wagombea watoe taarifa  kwa wana habari ili habari yao iweze kurushwa tutajuaje bila kutoa taarifa?
Balile

Post a Comment

0 Comments