JAMII YATAKIWA KUACHA USHABIKI WACHAGUE VIONGOZI WENYE SERA NZURI

 


📌NA HAMIDA RAMADHANI

 

JAMII imeshauriwa kuacha ushabiki usio na tija hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu Oktoba  2020 na  imetakiwa kuchuja na kuangalia sera bora zinazotolewa na wagombea .

 

Hayo yamesemwa leo na askofu Julius Bundala Wa kanisa  la Pentecostal  Holliness Association Mission lilipo kata ya Makole jijini hapa  wakati akifungua semina ya kina mama ya  siku nne kanda ya Kati yenye lengo  la kujifunza neno la Mungu,malezi ya familia, maisha ya ndoa, na ujasiriamali. 

Sasa hivi kumekuwepo  na ushabiki mkubwa hasa kwenye vyama vya siasa na kwenye vyama  vya mipira  kwa maana ushabiki wa namna hiyo utatupelekea nchi yetu kuingia katika machafuko.

Askofu Julius Bundala .

Aidha amesema kama   waliweza  kufunga na kuomba  kwa kipindi cha janga la Corona wana imani hata mchakato wa uchaguzi  wataenda kuombea taifa ili wapatikane  viongozi  walio  Bora. 

Tunatakiwa kuijiombea na kuwaombea viongozi wetu wanaokuja  kutuongoza wapite Kwa amani  nchi yetu ibaki na amani kwani pasipo amani hakuna maisha wananchi jiandaeni kupiga kura

Sambamba na hayo Askofu Bundala amewataka wanawake wajiamini  na waache ile dhana potofu ya kusema mwanamke  ni kiumbe dhaifu

Post a Comment

0 Comments