📌HAMIDA RAMADHANI
JUMUIYA ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) wamelalamikia kitendo cha wafanyabiashara wa Kichina kuingilia soko kuuza bidhaa zinazouzwa na wazawa
Aidha jumuiya hiyo imesema Wachina hao wanafanya biashara za kichuuzi ambazo zinafanywa na wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama Wamachinga hivyo kufanya mazingira ya Biashara kwa wazawa.
Akizungumza Jijini hapa katika mkutano wa wenyeviti na makatibu wa jumuiya hiyo Mwenyekiti wa JWT Silva Kyando alisema kuwa Wachina hao wanafanya mazingira ya Biashara kwa Wamachinga hususani wa Kariakoo kuwa magumu
Unajua Wachina kule kwao wanapata mikopo yenye riba nafuu kuliko sisi hivyo wakileta.biashara hapa chini Wana uwezo wa kuuza bei ya chini kuliko mfanyabiashara mzawa, hiyo inaua soko la Watanzania.
Silva Kyando
Amesema kuwa Wachina Kule.kwao wanapewa mikopo yenye yenye riba kuanzia asilimia 6 Hadi asilimia 5.5,wakati mikopo inayotolewa hapa nchini ni asilimia 20 hadi 40.
Aidha Kyando amesema kuwa Wachina hao wamekuwa wakilindwa na.Mamlaka husika hata wakipeleka malalamiko yao hayasikilizwi hivyo wanajikutaa wanaishi katika nchi yao Kama watoto Yatima.
Tunawapenda Wachina ni marafiki zetu wa muda mrefu,lakini hatutaki kuingiliwa soko letu ,wao ni wawekezaji siyo kuja kufanya Biashara ambazo Wamachinga.wanafanya. Kyando
Mbali na hilo Mwenyekiti huyo amesema kuwa kutokana na.mazingira ya kulindwa Wachina.hao wamekuwa wakwepaji Kodi wakubwa kwani Kuna wakati wanashusha makontena hakuna risiti za EFD Wala leseni hivyo wanajikutaa wakiuza kwa faida kubwa.
Mwenyekiti huyo amesema Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli ni sikivu .wanaamini Changamoto ya Wachina itafanyiwa kazi.
Aidha mbali na Changamoto ya Wachina Mwenyekiti huyo amesema tozo ya Service levy ni kero kubwa kwa Wafanyabiashara hivyo wanaomba Serikali ifute kwani wao siyo walengwa.
Kyando pia aliitaka Serikali kutumia hekima kuwatafutia maeneo maalum ya kufanyia Biashara Wamachinga kuliko kupanga bidhaa za mbele ya maduka.
Unakuta Mmachinga kapanga bidhaa zake mbele ya duka ambalo na lenyewe lina uza bidhaa ileilei hivyo wanawazibia riziki wenye maduka kwani wao wanauza kwa bei ya chini.
Silva Kyando
Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la
Biashara la Taifa Dkt. Godwin Wanga amesema Serikali ipo pamoja na
wafanyabiashara hao, ambapo aliahidi Changamoto hizo zitapelelwa sehemu husika.
0 Comments