MBUNGE TABASAMU KUBEBA KILIO CHA WAKULIMA WA PAMBA

 


📌HAMIDA RAMADHANI

MBUNGE wa Jimbo la Sengerema Tabasamu Mwagao (CCM) amesema atatumia vikao vya Bunge kulirudisha zao la Pamba katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa kuhamasisha usamabazaji wa mbegu za zao hilo.

Tabasamu ambaye  anaingia Bungeni katika kipindi cha kwanza aliongea hayo hivi karibuni mara baada ya kuapishwa  kiapo cha uaminifu katika hafla iliyofanyika Bungeni Jijini hapa.

Mimi naingia Bungeni kwa mara ya kwanza lakini nikiwa na vipaumbele vyangu, ambavyo la kwanza ni Pamba, nitahakikisha mbegu za Pamba zinasambazwa katika Mikoa ya kanda la Ziwa ili uzalishaji uongezeke.
Tabasamu Mwagao 

Aidha Tabasamu alisema ili zao la Pamba liweze kulimwa kwa wingi Serikali inatakiwa kuweka mfumo madhubuti katika kusambaza mbegu ambazo wakulima wengi watazipata kwa urahisi.

Kipindi cha nyuma Pamba ilikuwa ikilimwa katika Mikoa zaidi ya 16 lakini baadae pamba iliharibiwa kuanzia katika usambazaji wa mbegu, tatizolilianzia hapo.
Tabasamu Mwagao 

Aidha Mbunge huyo alisema kipaumbele chake kingine ni uboreshaji wa miundo mbinu ya maji ambapo alisema katika jimbo lake Wananchi wake wana shida ya maji.

Vilevile Mbunge huyo alisema akiwa Bungeni hapo atahakikisha anawasilisha tatizo la uhaba wa madarasa ya Shule za Msingi na Sekondari pamoja na Chuo cha Ufundi.

Mbunge huyo alisema atahakikisha anatumia vikao vya Bunge hilo la 12, kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili Wananchi wa jimbo la Sengerema bila kujali itikadi zao za Vyama au dini.

Mimi ni mtumishi wao, hivyo sitajali itikadi zao za Vyma, dini au kabila,niwatumikia Wananchi wa jimbo langu kwa usawa na kuwaletea maendeleo,nimekuja Bungeni kupiga kazi.
Tabasamu Mwagao 

Mbunge huyo alisema hata kama yeye ni wa CCM lakini hata kaa kimya kuhofia kuonekana mbaya,linapotokea suala la kuwasemea Wananchi wake atasema kwa maslahi ya Serikali

 

Post a Comment

0 Comments