MPWAPWA WATAKIWA CHANGAMKIA FURSA ZAO LA KOROSHO

 


📌STEPHEN NOEL (MPWAPWA). 

WANANCHI wa wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma  wametakiwa kuchangamkia fursa ya  upandaji wa zao la korosho ambalo linatarajiwa kuwa mkombozi wa uchumi wa wilaya hiyo na kukuza kipata kwa mtu moja moja. 

 Akizungumza na CPC Blog Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Jabir Shekimweri (Mzee wa Korosho )amesema kuwa tangu waanze kuhamasisha zao hilo mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa hivyo anawataka wale ambao bado wanajiuliza uliza wachangamkie fursa hiyo.

Shekimweri amesema  Serikali haitoacha kuhamasisha zao la korosho ambalo ni zao la kimkakati katika wilaya ya Mpwapwa ili kuinua uchumi wa wananchi.

Ukweli kuanza kitu kipya kinachangamoto zake wapo waliotikia toka mwanzo na wengine wanasita sita hivyo wakioshaona wenzao wamenufaika ndo na wao watajiingiza katika kilimo hicho.
Jabir Shekimweri

Aidha Shekimweri amewaagiza maafisa ughani na viongozi wote ngazi ya Kata na vijiji  kuhamasisha upandaji wa korosho katika kipindi hiki cha mvua. 

Kwa upande wake  afisa kilimo anaeshughulikia zao la Korosho wilayani Mpwapwa  Edson Kileo  amesema, tafiti zinaonyesha kuwa hali ya hewa ya wilaya ya Mpwapwa ni rafiki kwa zao la korosho na linafanya vizuri. 

Zao hili hustawi vizuri sehemu zenye mvua ya wastani kiasi cha milimita 800 mpaka 1,600 kwa mwaka kwa wilaya ya Mpwapwa ndicho kiasi cha mvua kinachoweza kupatikana kwa mwaka
Edson Kileo 

Aidha ameongeza kuwa korosho ni zao la kimkakati katika mikoa ya kanda ya Kati ambalo litaweza kubadilisha maisha ya wananchi wengi wa Mpwapwa  na uchumi wa wilaya kwa ujumla.

Mmoja wa wakulima wa zao hilo Suzana Mosha amesema kwa sasa wameanza kuvuna mavuno ya awali ya zao hilo na linaonyesha kufanya vizuri. 

Naye Jemsi Senyegalo amesema pamoja na wananchi kuitikia kwa wingi upandaji wa zao hilo idara ya kilimo inapaswa kushughulikia changamoto za  upatikanaji wa viwatirifu kwa wakulima ili wavutiwe kujiingiza katika kilimo cha zao la korosho. 

 

 

Post a Comment

0 Comments