TUNATAFUTA UFUMBUZI WA UPUNGUFU WA SUKARI.

📌NA MWANDISHI WETU.

WAZIRI, wa Kilimo Prof.Adolf Mkenda amesema Serikali inatambua mchango mkubwa wa viwanda vya ndani kuongeza uzalishaji ambapo katika kipindi cha miaka mitano ya Serikali ya awamu ya tano ya Dk. John Pombe Joseph Magufuli uzalishaji wa sukari umeongezeka kwa 78.3 %(kutoka tani 295,775 mwaka 2015/2016 hadi tani 377,527 zinazotarajiwa kuzalishwa msimu wa 2020/2021).


 Mafanikio haya ya kuongezeka kwa uzalishaji ni matokeo ya utekelezaji wa Sera na Mikakati ambayo Serikali imeweka kuhakikisha wazalishaji wana mazingira mazuri ya wazalishaji kufanya upanuzi wa mashamba na wakulima kuongeza tija.

Prof.Mkenda ameongeza kusema
Uzalishaji wa sukari kwa mwaka nchini ni wastani wa tani 300,000 ambapo katika msimu wa mwaka 2020/2021 jumla ya tani 377,527 za sukari zitazalishwa kutoka kwenye viwanda  vilivyopo vya Kilombero Sugar Company Ltd, Mtibwa Sugar Estate, Kagera  Sugar Ltd, TPC  Ltd na Manyara Sugar Ltd.

" Kwa ujumla mahitaji ya sukari nchini kwa matumizi ya kawaida na viwandani ni tani  655,000 kwa mwaka, ambapo katika hizo tani  490,000 zikiwa na ziada (buffer stock)  ya tani 70,000 sawa na mahitaji ya miezi miwili ni sukari ya matumizi ya kawaida na tani 165,000 ni  matumizi ya viwandani" alilsitiza Prof .Mkenda

Waziri huyo wa Kilimo alisema Kutokana na uzalishaji huo , sukari inayozalishwa nchini haitoshelezi mahitaji ya soko la ndani na hivyo Nchi huagiza wastani wa tani 40,000 za sukari ya matumizi ya kawaida (Gap Sugar) kufidia pengo la mahitaji halisi ya sukari nchini kwa matumizi ya kawaida.

Prof. Mkenda alitaja mikakati ya kuongeza uzalishaji sukari kuwa ni kuwapatia wakulima mbegu bora ya miwa, kujenga miundombinu ya umwagiliaji na kuhakikisha viwanda vya sukari nchini vinachakata miwa yote inayovunwa na wakulima hapa nchini.

Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda (katikati) akiongea na waandishi wa habari leo ofisini kwake Dodoma kuhusu mikakati ya serikali kuhakikisha miwa ya wakulima wote inachakatwa na viwanda vya ndani ili kuondoa upungufu wa sukari nchini. Wengine pichani ni Katibu Mkuu Kilimo Bw. Gerald Kusaya( kulia) na kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Sukari Tanzania Bi. Mwamini Malemi

Post a Comment

0 Comments