LUKUVI AAGIZA WAKUU WA MIKOA,WILAYA KUTATUA MIGOGORO

 


📌DOTTO KWILASA

SERIKALI  imewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya kufuatilia kwa ukaribu  migogoro ya ardhi na kuipatia ufumbuzi bila kusubiri viongozi wa ngazi ya kitaifa.

Waziri  wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Wiliam Lukuvi  amesema hayo wakati akizungumza na wadau wa Ardhi katika mkoa wa Dodoma katika ukumbi wa mikutano uliopo kwenye ofisi za mkuu wa mkoa.

Amewataka viongozi hao kuwajibika na si kusubiri viongozi wakubwa wafike waanze kusikiliza na kutatua migogoro wakati viongozi wa mikoa wa wilaya wapo itakuwa ni jambo la aibu,  ni vyema mkaanza ninyi itasaidia kupunguza migogoro ya ardhi kwa asilimia 90.

Amesema serikali ina mpango wa kuanza kuwasajili madalali wa ardhi nchi nzima ili wafanye kazi kwa weredi huku wakilipa kodi

Hakuna kitu kinamuumiza mwananchi wa kawaida kama migogoro ya ardhi hivyo lazima viongozi  wa mikoa na wilaya katika maeneo yenu kuhakikisha tunalinda rasilimali za maskini hasa ardhi

 

Pamoja na hayo amesema Jiji la Dodoma linatakiwa liwe la kisasa ambalo halina migogoro ya ardhi ili wananchi wake wajenge nyumba kwa kufuata utaratibu wa eneo husika ikiwa ni pamoja na kuendeleza mji kwa kujenga nje kidogo ya maeneo ya mijini.

 Waziri Lukuvi pia ameagiza uongozi wa jiji la Dodoma kuanza kutoa hati kwa njia ya mtandao hiyo itasaidia kupunguza misongamano ya watu na kuokoa muda kwenye kufatilia hati zao.

"Ningependa viongozi wa mkoa wajishughulishe sana kusikiliza kero za ardhi  mkoa wa Dodoma wameanza ningependa mikoa yote Tanzania iige ianze kusikiliza kero pamoja na kuzia ujenzi holela wa makazi," ameeleza

Licha ya hayo amewataka Wenyeviti wa Serikali za Mitaa  wa Mijini kuacha kujihusisha kwenye masuala ya kuuza ardhi bali shughuli hizo zitasimamiwa na wakurugenzi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Antony Mtaka amesema katika kuhakikisha wanatekeleza agizo la Waziri huyo wa Ardhi  ,Ofisi yake imetenga Siku 10 za kusikiliza  kesi za migogoro ya ardhi  kuanzia Julai 5 mwaka huu katika ukumbi wa jakaya kikwete.

Mtaka amesema katika siku hizo wametenga Siku tatu kwa ajili ya kusikiliza wananchi na kupokea malalamiko yao huku siku  saba zitakuwa kwa ajili ya kufika kwenye maeneo yenye migogoro.

"Tunaelekeza nguvu kutatua  migogoro ya ardhi hali hii  itasaidia  Wananchi kuishi kwa amani ,katika kutatua kero hiyo wananchi wafike na nyaraka zao zote na masharti ya wataaalamu wa afya yatazingatiwa kuhakikisha wanajikinga na maambukizi ya virusi vya Corona,"amesema na kuongeza;

Tunataka kuona Jiji la Dodoma linafanana  na majiji mengine duniani ambako hakuna migogoro ya ardhi, hivyo wananchi watatakiwa kufika mapema kuanzia saa moja asubuhi

 

Kutokana na hayo  Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Godwin Mkanwa amempongeza Waziri wa Ardhi kwa kuendelea kupambana dhidi ya migogoro ambayo ilikuwa imekithili na kusababisha baadhi ya shughuli za maendeleo kukwama.

Amesema migogoro ya ardhi inawavunja moyo  wawekezaji  na kuwataka wananchi kuzingatia utaratibu wa mipango miji ili jiji liwe la kisasa zaidi.

"Katika kutekeleza majukumu nawashauri watumishi wa serikali wajipange kusikiliza kero za wananchi kwasababu ni maagizo aliyoyatoa Rais Samia Suluhu Hassan ndani ya chama na serikali kwa ujumla,"amesema

Post a Comment

0 Comments