MTAKA ATAKA JAMII ISISUBIRI KUSUKUMWA KUJIKINGA CORONA

                      

📌DOTTO KWILASA

 

MKUU wa mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka amesema Jamii ina jukumu la kujilinda yenyewe na kuwalinda wengine dhidi ya ugonjwa wa COVID-19  bila kusubiri kusukumwa.

 Mtaka amesema hayo  kwenye Mkutano wake na Waziri wa Afya na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wakati akitoa mwelekeo wa njia wanazochukua kama mkoa katika kudhibiti maambukizi ya corana awamu ya tatu uliofanyika katika hospitali ya rufaa ya mkoa.

Akiongea katika mkutano huo,Mtaka amesema,uhai wa mtu sio Mali ya serikali hivyo ni jukumu la kila moja kuhakikisha anajilinda kwa kunawa mikono kwa maji safi tiririka na sabuni,kuvaa barakoa na kutumia vipupuzi.

Serikali ilishatoa miongozo mbalimbali ya kujikinga na janga la Corona lakini watu bado wanahoji kuitaka Serikali kutoa miongozo,mnataka miongozo gani hiyo!?

Mtaka,RC Dodoma

Pamoja na hayo Mtaka ameeleza miongozo na hatua  kadhaa ambazo Mkoa wa Dodoma umeanza kuzifuata Katika kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa huo  kwamba wao  kama mkoa wamedhamiria kuanza na maeneo ya stendi,sokoni,minadani na sehemu zote zenye mikusanyiko.

Amesema,kulingana na mabasi ya abiria kujaza wasafiri ,  ipo haja ya kuboresha miundombinu hiyo  ili kuendana na hali ilivyo ambao kila chombo Cha usafiri kitatakiwa kuwa na idadi ndogo ya abiria kwa kila safari kuepusha maambukizi. 

"Wasafirishaji wa abiria mnatakiwa kuzingatia maeleko yote yanayotolewa na Wizara ya afya,hampaswi kusimamisha abiria ndani ya gari na hili tunaomba wafanya biashara wa magari mtuelewe vizuri," amesema Mkuu huyo wa Mkoa wa Dodoma.

 Kutokana na hayo amewataka wasafiri  wote Mkoani hapa  kufuata taratibu za afya kwa kuhakikisha wanakuwa mabalozi wa usalama wao kwa  kuachiana  hatua moja Kati ya mtu na mtu na kuvaa barakoa kila wanapokuwa safarini.

”Hatuwezi kuzuia watu wasisafiri,hili  haliepukiki sehemu yeyote hivyo ni vyema watu wakawa na mazoea ya kukubali kusafiri bila kubanana kwenye Vyombo vya usafiri,"amesema.

Kuhusu  Masoko,Mkuu huyo wa mkoa ameagiza Wafanyabiashara wa Masoko yote  yaliopo mkoani Dodoma,kuvaa barakoa kila wanapohudumia wateja wao ikiwa ni pamona na watoa huduma  waliomo ndani ya eneo la solo  kuhakikisha wanatoa huduma wakiwa wamevaa barakoa .


 Licha ya hayo ametoa maelekezo kwa Wafanyabiashara wa minada yote Mkoani hapa kuhakikisha wanafuatilia lwa umakini kanuni zote za afya kwa kuwakinga wanaowahudumia.

"Hatuwezi kufunga minada kwa sababu za ujinga wa wachache,kila mmoja anajua namna ya kujikinga,niwaambie tu kuwa mnada huu ndiyo utakuwa wa mwisho kwa ninyi kuuza bidhaa zenu bila kufuata Sheria za kujikinga na Corona,minada inayofuta baada ya leo tunataka kukuta kila mfanyabiashara maevaa barakoa,na hii ni lazima na sio ombi,"amesisitiza Mtaka.

 Pia amehimiza Uongozi wa minada yote kuhakikisha minada inakuwa na huduma za maji tiririka,sabuni na vitakasa mikono kuwezesha wananchi wanaopata huduma kupata maji kwa urahisi kwa ajili ya kujitakasa.

Licha ya hayo ametoa wito kwa jamii kufika katika vituo vya kutolea huduma za afya mara wanapoona dalili za ugonjwa huo ili kubaini  huku akiwatahadharisha kuepuka kujifukiza bila utaratibu.

 Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma, Meja Mstaafu Salingo  Risasi amesema VIONGOZI wa Dodoma wamekuwa na ushirikiano mkubwa na Chama cha Mapinduzi (CCM)  katika mapambano hayo ya Corona na wamekuwa wakikutana kwenye vikao katika kujadili namba ya wananchi kuweza kupata elimu ya kujikinga na ugonjwa huo.

 Meya ya jiji la Dodoma Profeda Devis Mwamfupe amesema janga hili ni janga la kiduni hivyo inatakiwa kila mmoja kupambana kwa ajili ya kuokoa maisha.

"Nipende kusema kuwa suala la Ugonjwa unaotokana na kirusi cha Covid -19 awamu ya tatu ni ugonjwa unaolikumba taifa kutokana na hali hiyo ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha analinda afya yake bila kusubili maelekezo ya kutoka ngazi ya taifa" alisema mwamfupe.

Kutokana na umuhimu huo,Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii  Njisia Wazee na Watoto Dkt Dorothy Gwajima ametumia nafasi hiyo kuwata wakuu wa Mikoa na wakuu wa Wilaya nchini kuzingati miongozo 16 ya kujikinga na kupambana na ugonjwa wa Corona (CORONA 19 awamu ya 3).

Dk.Gwajima  Kila mkoa unapaswa kujipambanua kuona namna ya kuwashawishi wananchi wake kuwa makini na ugonjwa huo hasa Katika kipindi hiki ambacho   wagonjwa wa Corona wameanza kuonekana katika hospitali zilizopo hapa nchini.

"Kwa  maana hiyo   kama wilaya au mkoa tuone sasa tumejipanga vipi kukabiliana na janga hilo kubwa linaloitesa dunia zima.

Nimefurahi kuona mmejipanga katika mapambano ya Corona kila sehemu lakini niwe muwazi nimekuwa nikipata Maoni mengi kwa wananchi waishio pembezoni huko vijijini elimu ya kujikinga na kupambana na Corona haiwafikii,jitahidini kwa hili
Dkt Gwajima.

 Mbali na hayo ameongeza; " Sasa natoa maelekezo kuanzia jumatatu wizara ya afya tutakuwa na Rejesta itakayo onyesha kila Halmashauri imefanya vipindi vingapi hasa kwenye vyombo vyetu vya habari vya ndan vya kuelimisha wananchi kujikinga kwa kunawa mikono ,kuvaa barakoa, kutumia vipupuzi na tuepuke mikusanyiko isiyo ya lazima" amesema 

Amesema vita ya ugonjwa wa Corona  itakoma na kushindwa ikiwa wananchi watakubali kubadili tabia na kufuata miongozo inayotolewa na wizara ya Afya.


 Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma, Meja Mstaafu Salingo  Risasi amesema Viongozi wa Dodoma wamekuwa na ushirikiano mkubwa na Chama cha Mapinduzi (CCM)  katika mapambano hayo ya Corona na wamekuwa wakikutana kwenye vikao katika kujadili namba ya wananchi kuweza kupata elimu ya kujikinga na ugonjwa huo.

 "Nipende kusema kuwa suala la Ugonjwa unaotokana na kirusi cha Covid -19 awamu ya tatu ni ugonjwa unaolikumba taifa kutokana na hali hiyo ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha analinda afya yake bila kusubili maelekezo ya kutoka ngazi ya taifa" amesema.

 

Post a Comment

0 Comments