WAZIRI UMMY AWAPELEKA POLISI WATENDAJI WA KIJIJI,KISA?MICHANGO

 


📌NTEGENJWA HOSSEA

WAZIRI TAMISEMI Ummy Mwalimu amewakabidhi Mikononi mwa Polisi viongozi wa Kijiji cha Nyamililo Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mkoni Mwanza kwa kuchangisha wananchi michango bila Kibali cha Mkuu wa Wilaya.

Waziri Ummy amechukua hatua hiyo wakati wa ziara yake Wilayani humo ambapo alitembelea Zahanati ya Nyamililo kukagua maendeleo ya ujenzi.

Akiwa Zahanati ya Nyamalilo,Waziri Ummy amebaini kuwa licha ya TAMISEMI kupeleka fedha za kukamilisha Zahanati hiyo Shilingi Mil 50 ambazo kwa hali ya Zahanati ilivyokua ingekamilika na fedha kubaki lakini Viongozi hao wa Kijiji waliendelea kuwachangisha wananchi sh 9,500 kwa Kaya kwa madai wanakamilisha zahanati hiyo.



Viongozi wa kijiji cha Nyamililo wakiwa mikononi mwa polisi kwa tuhuma za kuchangisha michango bila kibali.

Wakiwasilisha malalamiko yao Wananchi hao wamesema waliposhindwa kutoa michango hiyo walichukuliwa Kuku, mbuzi na wengine hata Baiskeli kitendo ambacho hawakukifurahia na wao wanapenda maendeleo lakini viongozi hao wa vijiji wamezidisha michango.

Akiwasilisha Taarifa ya Ukamilishaji wa Zahanati hiyo Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dr. Saumu Kumbisaga amesema ktk mil 50 zilizopokelewa wametumia sh Mil 33.2 na bakaa ni mil 16.7.

Kazi zilizofanyika ninupigaji wa ripu nje na na ndani, kukazia paa, uwekaji wa Fremu za madirisha na milango, uwekaji wa Gypsum board, kumwaga Jamvi, uwekaji wa vigae na ujenzi wa ukuta wa varander 

Dr. Saumu.

Sanjari na hilo,Waaziri Ummy amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema kumsimamisha kazi Mtendaji wa Kijiji cha Nyamiliho Mariam Mgunda kwa kuratibu zoezi la kuchangisha wananchi fedha.



Post a Comment

0 Comments